• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

.

Imetolewa: July 16th, 2021

MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Martine Shigela, amewataka Maafisa Maendeleo ya Jamii wa Halamshauri zote zilizopo Mkoa wa Morogoro kutoa elimu ya kutosha ya Bima ya CHF iliyoboreshwa (iCHF) kwa Wananchi.

Hayo ameyazungumza Julai 16, 2021 katika Mkutano wa Nusu Mwaka wa Tathimini ya Mkataba wa Lishe na Bima ya Afya ya Jamii (ICHF).

Akizungumza na waashiriki katika Mkutano huo, RC Shigela, amesema zipo changamoto katika Mkoa wa Morogoro kwenye muitikio wa Wananchi kukata Bima ya afya ya CHF iliyoboreshwa .

RC Shigela, amewaagiza Maafisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri zote Mkoa wa Morogoro kwa kushirikiana na Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi kuona njia mbalimbali za kuongeza idadi ya wananchi katika mfuko wa bima ya afya ya CHF iliyoboreshwa.

Amesema kwa Mkoa wa Morogoro umefikia asilimia 9.4 ya zoezi la uandikishaji wa Bima za CHF iliyoboreshwa ambapo kwa malengo ya kufikia mwaka 2025 Mkoa wa Morogoro unatakiwa kufikia asilimia 34%.

Amesema kuwa kati ya asiliia 9.4% za waliojiandikisha katika mfuko wa Bima ya afya ya CHF iliyoboreshwa ni asilimia 3.4% ya wananchi ambao ndio wanapata huduma ya bima ipasavyo.

‘’Bado Mkoa wetu wa Morogoro tunachangamoto kubwa ya bima hii ya CHF iliyoboreshwa , asilimia ya wanachama wetu tuliowaandikisha hawapati huduma kama inavyostahili, kumekuwa na malalamiko sana katika upande huu wa bima, wengi wanalalamika dawa hakuna wakati sehemu nyengine zipo, Maafisa Maendeleo nyie ni watu muhimu sana katika eneo hili, na muna jukumu hilo na ndio maana mmesomeshwa na Serikali tupe huo utaalamu hakikisheni idadi ya wanachama wanaongezeka’’Amesema RC Shigela.

Katika hatua nyengine, amepiga marufuku Watumishi katika Vituo vya afya wanaotumia fedha za huduma zinazotolewa na wagonjwa Hospitalini kuzifanya ni mali yao.

Amesema kuwa Katika Vituo vya afya kumekuwa na mchezo mchafu ambao baadhi ya watumishi wamekuwa wakihudumia wagonjwa wasiokuwa na bima kuchukua fedha bila kuingiza katika mfumo wa malipo.

‘’Nitoe rai kwa waatumishi wa namna hiyo , utakuta baaadhi ya Vituo vya afya idadi kubwa ya wanaohudumiwa wamekuwa wakiwaandikisha katika matibabu ya huduma za msamaha , huku fedhaa za wagonjwa wakizitumbukiza mifukoni , tutakao wabaini tutachukua hatua kubwa za kisheria , ni bora tubakie na watumishi wachache kuliko kubaki na rundo la watumishi wanaotuhujumu’’Ameongeza RC Shigela.

Kwa upande wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Bi. Mariam Mtunguja, amewaomba wataalamu pamoja na wadau wa afya wasirudi nyuma kwani suala la lishe linatakiwa lipewe kipaumbele.

Bi. Mtunguja, amesema kuwa tofauti kubwaa ya watoto kupishana kiakili kinatokana na kupata lishe bora.

‘’Mtoto akipata virutubisho vya kutosha anakuwa na akili nyingi, sasa ni jukumu letu kuhakikisha suala la lishe linakuwa agenda mama katika vikao vyetu ili tutengeneze vizazi vyenye akili kwa ajili ya Mkoa wetu wa Morogoro na Taifa kwa ujumla’’ Amesema Bi. Mtunguja.

Amesema kuanzia mwaka wa fedha wa 2021/2022 vipimo vya utambuzi wa lishe vitaapimwa kuanzia ngazi ya Kata.

Katika Mkutano wa nusu mwaka wa Tathimini ya Mkataba wa Lishe na Bima ya afya ya Jamii (iCHF) , umehudhuriwa na Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Wataalamu wa Halmashauri, Wataaalamu wa Lishe ngazi ya Mkoa na Halmashauri pamoja na wadau wa lishe Mkoa na Halaamshauri zote.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO A UPANGA VYUMBA VYA OFISI NA MAENEO MBALIMBALI YALIYOPO MOROGORO MJINI March 19, 2025
  • TANGAZO LA KAZI YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU, DEREVA NA MTENDAJI WA KIJIJI July 15, 2024
  • TANGAZO LA RASIMU July 25, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 12, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEEA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO,MAAGIZO YATOLEWA

    April 11, 2025
  • KATIBU TAWALA MKOA WA MOROGORO AENDELEZA KAMPENI YA JISOMESHE NA MKARAFU

    March 14, 2025
  • "BAINISHENI VYANZO VYA MAJI NA MVILINDE" MHE.KASSIM MAJALIWA MAJALIWA

    March 05, 2025
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.