• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Jafo aitaka Tume ya Utumishi wa Walimu Kutatua Changamoto za Walimu

Imetolewa: May 25th, 2020

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Selemani Jafo ameitaka Tume ya Utumishi wa Walimu kutatua changamoto na malalamiko ya walimu ikiwemo kubadilishwiwa mishahara baada ya kujiendeleza kielemu pamoja na manung’uniko mengine ili kuwatia moyo walimu katika kutimiza majukumu yao.

Kauli hiyo ameitoa  jijini Dodoma wakati wa kuteuliwa na kuapishwa kwa wajumbe wa Tume ya Utumishi wa Walimu .

Mhe. Jafo amesema kuwa Tume hiyo ndani ya wiki moja ikafanyie kazi malalamiko ya muda mrefu ikiwemo walimu kuchelewa kupandishwa madaraja baada ya kujiendeleza pamoja na kushughulikia mashauri ya rufaa ili walimu waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Amesisitiza  kuwa Tume hiyo inatakiwa kufanya kazi kwa weledi wa hali ya juu hasa katika kushughulikia Ajira na Usajili, kupandisha madaraja, kubadilisha cheo walimu waliojiendeleza kimasomo pamoja na kusimamia maadili na nidhamu ya Walimu.

“Pamoja na mazingira magumu na changamoto naomba nikiri kwamba Tume ya Utumishi wa Walimu imefanya kazi kubwa tangu ianzishwa mwaka 2016 hadi sasa nendeni kaendeleze kasi ile ile mkawe sikio la walimu na kusimamia nidhamu ya walimu ili kuleta utendaji bora katika kutekeleza majukumu yao”, amesema Mhe. Jafo.

Aidha Mhe. Jafo ameitaka Tume hiyo kufanya kazi katika kanuni, miongozo na Taratibu zilizopo ili kuleta uwajibikaji katika shughuli za walimu hapa nchini.

Aidha mhe. Jafo ametoa wito kwa Mwenyekiti wa Tume hiyo Prof. Willy Lazaro Komba kutoa ushirikiano kwa wajumbe wake ili kuweza kufanyikisha shughuli za utendaji katika ubora unaohitajika na walimu wanao wahudumia.

Wakati huo huo  Mhe. Jafo amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa maono yake juu ya kupambana na janga la Corona kwa kutozuia shughuli za watanzania ila kuwataka kuchukua taadhali na wananchi kuendelea na uzalishaji wao katika kutafuata kipato chao.

“Natoa rai kwa watanzania kuendelea kujifukizia (kupiga nyungu) kwa awamu ya pili ili kuimarisha afya zao zaidi na kupambana na kupambana na corana kwani vita hii haichagui siraha” alisisitiza Jafo.

Naye Mwenyekiti wa Tume hiyo Prof. Willy Lazaro Komba akitoa neno la shukurani amesema kuwa watatekeleza majukumu yao ipasavyo ili wanao wahudumia kupata huduma bora wanazotarajia kutoka kwao.

“Tuko tayari kuanza kazi ili kuwatumikia tunao waongoza na kufanikisha ubora katika shughuli za Walimu kote Nchini” ameeleza Prof. Komba.

Prof. Komba ametoa wito kwa wajumbe kutoa ushirikiano wa kutosha katika kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.

Awali akitoa neno la ukaribisho Katibu Ofisi ya Rais, Tume ya Utumishi wa Walimu Bi. Winfrida Rutaindurwa alieleza kuwa tangu Tume ianze kutekeleza majukumu yake mwaka 2016 walimu 11,581 wameajiriwa, 14,507 walisajiliwa, 20,501 walithibitishwa kazini, 123,000 walipandishwa vyeo, 5,760 walibadilishwa vyeto baada ya kujiendeleza na walimu 20,316 wamestaafu na kuandikiwa vibali vya  kustaafu kazi.

Jufuatia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Joseph Magufuli kumteua Dkt. Willy Lazaro Mbuju Komba kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe Selemani Jafo kuteua na kuwaapisha wajumbe nane wa TSC.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO A UPANGA VYUMBA VYA OFISI NA MAENEO MBALIMBALI YALIYOPO MOROGORO MJINI March 19, 2025
  • TANGAZO LA KAZI YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU, DEREVA NA MTENDAJI WA KIJIJI July 15, 2024
  • TANGAZO LA RASIMU July 25, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 12, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEEA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO,MAAGIZO YATOLEWA

    April 11, 2025
  • KATIBU TAWALA MKOA WA MOROGORO AENDELEZA KAMPENI YA JISOMESHE NA MKARAFU

    March 14, 2025
  • "BAINISHENI VYANZO VYA MAJI NA MVILINDE" MHE.KASSIM MAJALIWA MAJALIWA

    March 05, 2025
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.