• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

RAS MOROGORO AZINDUA KAMPENI KUHAMASISHA ULAJI WA VYAKULA ASILIA MASHULENI

Imetolewa: January 19th, 2024

Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa amezindua kampeni ya kuhamasisha utoaji wa chakula cha mchana kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari Mkoani humo kwa kutumia vyakula vya asili vinavyopatikana kwenye maeneo husika.


Dkt. Mussa amezindua kampeni hiyo leo Januari 19, 2024 katika viwanja vya shule ya msingi Mtombozi iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro kwa lengo la kuhamasisha wazazi na walezi kuchangia upatikanaji wa chakula cha mchana kwa wanafunzi Mkoani humo.


Dkt.Mussa amesema Mkoa wa Morogoro umebarikiwa kuwa na aina mbalimbali za vyakula vya asili vikiwemo mashelisheli, mihogo, Viazi vitamu na ndizi huku hivyo haoni sababu ya wanafunzi kukosa chakula mchana na kuwataka wazazi kwa kushirikiana na Walimu kufanikisha upatikanaji wa vyakula hivyo kulingana na maeneo husika.


“...kuja kwangu leo hapa ni kuanzisha hii kampeni, si kwa hapa tu lakini kwa Halmashauri nzima na Morogoro nzima lazima tukubali kutumia vyakula vyetu vya asili tulivyokuwa navyo...” amesema Dkt. Mussa.


Aidha, Dkt. Mussa  ameeleza kuwa kukosekana kwa chakula shuleni kuna sababisha utoro na kushuka kwa ufaulu wa wanafunzi, hivyo ameuagiza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro kuhakikisha kuwa inapanda miche ya mashelisheli angalau miche miwili kwa kila shule za Wilayani humo.


Naye Afisa Lishe Mkoa wa Morogoro Bi. Salome Magembe amewashauri wazazi na walezi kuzingatia makundi matano ya vyakula Vikiwemo vyakula vya protini, wanga, Vitamini, mafuta na mboga mboga ili kupata mlo kamili kwa ajili ya kuboresha afya.


Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Ndg. Patrick Gwivaha amemshukuru Katibu Tawala kwa kuanzisha na kutulia mkazo kampeni hiyo ambayo itasaidia kupandisha kiwango cha ufaulu katika Halmashauri na kumhakikishia utekelezaji mzuri wa maagizo aliyoyatoa.


Katika kuhamasisha kampeni hiyo Dkt. Mussa ameahidi kuichangia shule ya msingi Mtombozi dagaa kilo 100 kwa ajili ya chakula kwa wanafunzi wa shule hiyo.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 10, 2025
  • TANGAZO A UPANGA VYUMBA VYA OFISI NA MAENEO MBALIMBALI YALIYOPO MOROGORO MJINI March 19, 2025
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • ORODHA YA WANAFUNZI WA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO AWAMU YA PILI 2018. September 07, 2018
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • SHILINGI MILIONI 538 NA LAKI NNE KUNUFAISHA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WALEMAVU

    June 20, 2025
  • MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI: MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 12, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEEA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO,MAAGIZO YATOLEWA

    April 11, 2025
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.