Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Selemani Jafo ameitaka Tume ya Utumishi wa Walimu kutatua changamoto na malalamiko ya walimu ikiwemo kubadilishwiwa mishahara baada ya kujiendeleza kielemu pamoja na manung’uniko mengine ili kuwatia moyo walimu katika kutimiza majukumu yao.
Kauli hiyo ameitoa jijini Dodoma wakati wa kuteuliwa na kuapishwa kwa wajumbe wa Tume ya Utumishi wa Walimu .
Mhe. Jafo amesema kuwa Tume hiyo ndani ya wiki moja ikafanyie kazi malalamiko ya muda mrefu ikiwemo walimu kuchelewa kupandishwa madaraja baada ya kujiendeleza pamoja na kushughulikia mashauri ya rufaa ili walimu waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.
Amesisitiza kuwa Tume hiyo inatakiwa kufanya kazi kwa weledi wa hali ya juu hasa katika kushughulikia Ajira na Usajili, kupandisha madaraja, kubadilisha cheo walimu waliojiendeleza kimasomo pamoja na kusimamia maadili na nidhamu ya Walimu.
“Pamoja na mazingira magumu na changamoto naomba nikiri kwamba Tume ya Utumishi wa Walimu imefanya kazi kubwa tangu ianzishwa mwaka 2016 hadi sasa nendeni kaendeleze kasi ile ile mkawe sikio la walimu na kusimamia nidhamu ya walimu ili kuleta utendaji bora katika kutekeleza majukumu yao”, amesema Mhe. Jafo.
Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road
Postal Address: 1880, Morogoro Tanzania
Telephone: +255 23 2935458
Mobile:
Email: ded@morogorodc.go.tz
Copyright © 2017 Morogorodc. All rights reserved.