• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WAZIRI MKUU,MHE. MAJALIWA KASSIM MAJALIWA, AMETEMBELEA ENEO LA MRADI WA KUZALISHA UMEME KATIKA MAPOROMOKO YA MTO RUFIJI - STIEGLERS GORGE.

Imetolewa: October 6th, 2018

Waziri mkuu wa Jamhuri ya muungano ya Tanzania ametembelea eneo unapojengwa mradi mkubwa wa kufua umeme unaotokana na maporomoko ya maji ya Mto Rufiji maarufu kama Stiglers gorge.

Waziri Mkuu ametembelea eneo hilo, alipokuwa katika ziara ya siku mbili Mkoani Morogoro na kuamua kutembelea na kujionea mwenyewe maandalizi ya ujenzi wa Mradi huo ambao upo mpakani mwa Wilaya ya Morogoro Mkoani Morogoro na Wilaya ya Rufiji Mkoani Pwani.

Baada ya kutembelea na kupewa maelezo ya maandalizi ya ujenzi mradi huo kuwa yamefikia asilimia 80 alieleza  kuwa mradi huo pamoja na malengo mengine unalenga kudhibiti uharibifu wa mazingira na siyo kuharibu mazingira kama ambavyo baadhi ya watu wanavyosema.

Awali waziri mkuu alipata maelezo ya maendeleo ya mradi toka kwa waziri wa nishati na madini Dkt.Medard Kalemani ambaye alisema kuwa:- Ujenzi wa barabara na ukarabati wa madaraja kufika eneo la mradi ( barabara ya kutoka Kibiti hadi na eneo la mradi na barabara ya kutoka Ubena Zomozi hadi eneo la mradi) umefikia asilimia 88.

Kazi ya kupeleka umeme katika eneo la mradi ( kV 33) kutoka Msamvu Morogoro kwa umbali wa kilometa 69. 2 imekamilika na kinachofanyika sasa ni kutandaza nguzo katika eneo la mradi.

Kazi ya kujenga miundombinu ya maji kwa ajili ya wafanyakazi watakaokuwa katika eneo la mradi imekamilika kwa asilimia 100.

Kazi ya kujenga na kupanua reli katika eneo la Fuga inatarajiwa kukamilika mwezi huu.

Kazi ya kukuza mawasiliano katika eneo la hifadhi inaendelea.

Katika taarifa yake Mh waziri wa nishati alisisitiza kuwa Matarajio ni kuwa shughuli zote zitakamilika ifikapo tarehe 10 mwezi huu.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa katika eneo la mradi wa umeme wa Rufiji (2100) alikagua eneo la mradi na pia alikagua ujenzi wa kituo cha reli ya Tazara eneo la Fuga kitakachotumika kushusha mizigo wakati wa utekelezaji wa mradi huo wa umeme.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO A UPANGA VYUMBA VYA OFISI NA MAENEO MBALIMBALI YALIYOPO MOROGORO MJINI March 19, 2025
  • TANGAZO LA KAZI YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU, DEREVA NA MTENDAJI WA KIJIJI July 15, 2024
  • TANGAZO LA RASIMU July 25, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 12, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEEA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO,MAAGIZO YATOLEWA

    April 11, 2025
  • KATIBU TAWALA MKOA WA MOROGORO AENDELEZA KAMPENI YA JISOMESHE NA MKARAFU

    March 14, 2025
  • "BAINISHENI VYANZO VYA MAJI NA MVILINDE" MHE.KASSIM MAJALIWA MAJALIWA

    March 05, 2025
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.