• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Hifadhi ya Kimboza

UTALII KATIKA MSITU WA HIFADHI WA KIMBOZA

Mahali ulipo

Msitu wa hifadhi wa Kimboza upo umbali wa kilomita 45 toka Morogoro Mjini.Msitu umezungukwa na vijiji vinne (4) vya Mwarazi, Changa, Kibangile naKilemela. Makao makuu ya hifadhi ya msitu ni kitongoji cha Kibungo chinikilichopo kijiji cha Mwarazi. Ukubwa wa msitu ni hekta zipatazo 405.

Kibao elekezi cha Msitu wa Hifadhi Kimboza- eneo la Kibungo chini

Asili ya neno Kimboza

Limetokana na neno la kabila la Kiluguru “Hotza” ikiwa na maana ya kupozamatatizo mbalimbali yakiwemo magonjwa na njaa. Hii ilitokana na msitu huukunufaisha vijiji jirani kwa kuwa na miti ya dawa, ukindu, na uwepo wa vyanzovingi vya maji kwa matumizi mbalimbali. Mboga za asili mfano delega, mlendana uyoga vinapatikana katika msitu huu kwa matumizi ya nyumbani.Ndani ya msitu wa hifadhi kuna miti ya matunda ya asili (milimili) ikiwa nichakula cha binadamu pamoja na ndege. Matunda haya yanaiva kwa mafungu(bundles) kama yanavyoonekana katika picha hapa chini:

Matunda aina ya milimili yanayofaa kuliwa na binadamu

Michikichi (Palm trees) – Mimea hii ni ya asili na hutoa matundayanayotumika kutengeneza mafuta ya mawese. Mafuta haya husaidiakung’arisha macho kwa watu wenye uoni hafifu. Mbegu za michikichizimeenea katika tarafa ya Matombo ambapo wakazi wake hukamua mafuta nakuuza kwa lengo la kujipatia kipato.

Mafuta ya mawese yakiwa kwenye ujazo tofauti kwa ajili yakuuzwa

Aidha Michikichi ni moja ya mimea asilia iliyoota kwa wingi na kutengenezamwonekano mzuri ndani ya msitu sambamba na kuhifadhi vyanzo vya maji.


Michikichi ikiwa ni moja ya uoto wa asili katika msitu waKimboza

Dawa za asili: 

Zipo dawa za kutibu magonjwa mbalimbali ndani ya msitu yakiwemo magonjwa ya tumbo, Malaria, meno na kuongeza nguvu za kiume.

Wanyama Adimu 

Katika msitu wa hifadhi wa kimboza kuna mjusi anayefahamika kwa jina maarufu Mjusi williamsi (Electric Blue Dwarf Gecko) na ambaye hapatikani sehemu nyingine duniani. Muda mzuri wa kumuona mjusi ni majira ya asubuhi kabla jua halijachomoza. Tofauti ya jike na dume ni kupitia rangi zao ambapo dume huwa na rangi ya blue na jike huwa na rangi ya kahawia kama wanavyoonekana katika picha hapa chini:

Mjusi Williams-Dume na Mjusi Williams-jike

Makazi ya mijusi ni kwenye mimea inayojulikana kwa jina la Kiswahili Mikongepori (Pandanus spp).

Baadhi ya Ndege wakiwemo hondohondo, njiwa na wanyama kama mbegaweusi na weupe, Dondoro, Mbawala, Funo na Nguruwe pori wanapatikanakatika msitu huu.Miti ya asili: miti ya asili yenye umri wa miaka 50 na zaidi inapatikana katika msitu wa hifadhi. Ipo mikangazi, mininga, mipululu, mivule na mininga maji

Pango la milango nane: Pango hili ni kivutio kwa kuwa na mfano wa milango yakuingilia, kutokea, sebule pamoja na vyumba vya kupumzika.

Moja ya mapango katika msitu wa hifadhi- Kimboza

Choka wahawi

Hili ni neno la kabila la waluguru ambapo eneo hili ni pango lililotumiwa nawazee wa kale kutoa adhabu kwa watu waliosadikiwa kuwa wachawi. Waliokirimakosa waliachiwa kwa sharti la kutokurudia tena kwa kula kiapo cha kimila.Eneo hili pia lilitumika kwa matambiko kwa kutumia mti ulioitwa Mtambika

Kibao elekezi ndani ya msitu wa hifadhi kuelekea maeneo yamatambiko

Dago la njiwa

Kwa maana ya pango la njiwa kwa lugha ya kiswahili ikiwa ni makazi ya njiwa na kanga. Ndege hawa huruka majira ya asubuhi kwenda kutafuta chakula na kurudi nyakati za jioni kwa ajili ya kulala.

Mtalii akiwa kwenye dago la njiwa

Ukanda wa Mimea vamizi: Ukifika msitu wa Hifadhi wa Kimboza utafanikiwakuona athari za mimea vamizi aina ya Misederea (Cedrela odorata) ikiwaimeshamiri na kuzuia kuota na kushamiri kwa miti ya asili (Allelopathic plants).Miti hii ina sifa ya kuwa na harufu kali inayozuia kushambuliwa na mchwa.

Miti aina ya misedera ikiwa imepukutisha majani

Vyanzo vya maji ya chumvi

Ndani ya msitu wa Hifadhi kuna vyanzo vingi vya maji kwa matumizi ya binadamuna viumbe hai wengine. Vijiji vinavyozunguka msitu wa hifadhi vinanufaika nauwepo wa maji safi na salama.


Moja ya chanzo cha maji kinachowanufaisha wananchi

Shughuli zinazofanyika

Safari za miguu kuanzia majira ya saa kumi na mbili asubuhi kwa lengo lakuona mijusi, ndege, wadudu na wanyama wengine. Kupiga picha namapumziko katika eneo maalum (camp sites) bila kuathiri mazingira ni moja yashughuli zinazofanyika katika msitu wa hifadhi.

Moja ya safari za miguu (Walking safari ) katika msitu wahifadhi - Kimboza

Moja ya banda la Mapumziko (Resting bandas) -Msitu wahifadhi kimboza

Muda mzuri wa kutembelea hifadhi: Kuanzia mwezi Mei hadi Septemba kwavile miezi iliyobaki ni ya mvua nyingi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 10, 2025
  • TANGAZO A UPANGA VYUMBA VYA OFISI NA MAENEO MBALIMBALI YALIYOPO MOROGORO MJINI March 19, 2025
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • ORODHA YA WANAFUNZI WA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO AWAMU YA PILI 2018. September 07, 2018
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI: MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 12, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEEA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO,MAAGIZO YATOLEWA

    April 11, 2025
  • KATIBU TAWALA MKOA WA MOROGORO AENDELEZA KAMPENI YA JISOMESHE NA MKARAFU

    March 14, 2025
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.