• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

IUCN YATAMBULISHA MRADI WA RESOLVE (NbS) HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO

Imetolewa: October 3rd, 2025

Shirikisho la Uhifadhi wa Mazingira Asilia Duniani (IUCN) leo Oktoba 3, 2025 wametambulisha Mradi wa RESOLVE NbS katika ngazi ya Halmashauri, pamoja na mmoja wa mbia katika utekelezaji ambaye ni CARE.


Mradi huo wa RESOLVE NbS (SULUHISHO) ni mradi wa Uhifadhi wa Mazingira kwa njia za Asili, ambapo vijiji vinne vya Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro vitanufaika. Vijiji hivyo ni Kisarawe na Milawilila vilivyopo Kata ya Tawa, pamoja na Amini na Kalundwa vilivyopo Kata ya Kinole.

Ukiwa unakwenda sambamba na kauli mbiu ya UHAI, USTAHIMILIVU na MAENDELEO, Mradi wa Suluhisho utakuwa wa miaka mitatu (2025–2027) na utajikita zaidi katika shughuli za; -


1. Kuwezesha wadau mbalimbali, hususan sekta binafsi, katika namna bora ya kupanga na kutekeleza masuluhisho asilia;


2. Kuimarisha uwezo wa maafisa wa halmashauri juu ya kupanga na kuingiza vipaumbele vya kuhimili mabadiliko ya tabianchi kwenye mipango na bajeti;


3. Kuhamasisha jamii juu ya utekelezaji wa kilimo mseto na kilimo bioanuai kwa kupitia mashamba darasa;


4. Kutengeneza au kuboresha mipango ya matumizi bora ya ardhi kutokana na kiwango cha uhitaji ukilinganisha na vijiji vingine vya mradi;


5. Kurejesha ikolojia za misitu, ardhi na mito zilizoharibiwa;


6. ⁠Kuboresha uwezo na mifumo ya jamii kwenye kuweka na kukopa (VSLA);


6. Kuboresha mifumo ya uuzaji wa mazao kwa kutumia vyama vya ushirika (AMCOS); na


7. Kutengeneza Mpango Mkakati wa kuhimili mabadiliko ya tabianchi na kukabiliana na maafa katika ngazi ya Wilaya.


Lengo kuu ni kuimarisha ustahimilivu wa watu na rasilimali dhidi ya athari za mabadiliko ya tabianchi kwa kutumia masuluhisho asilia.

Utekelezaji wa shughuli tajwa za Mradi, pamoja na nyinginezo, utahusisha wabia mbalimbali ambao ni CARE, WWF, EAMCEF, CAN na CEO Round Table (CEOrt), ambapo jumla ya Dola za Kimarekani milioni 5.3 zinatarajiwa kutumika.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 10, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI MOROGORO DC August 30, 2025
  • TANGAZO A UPANGA VYUMBA VYA OFISI NA MAENEO MBALIMBALI YALIYOPO MOROGORO MJINI March 19, 2025
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • Ufungaji wa Smart Board katika Shule za Secondary

    October 28, 2025
  • UTEUZI WA KUITWA KATIKA MAFUNZO JIMBO LA MOROGORO KUSINI NA MOROGORO KUSINI MASHARIKI.

    October 18, 2025
  • JARIDA MAFANIKIO HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO

    October 09, 2025
  • IUCN YATAMBULISHA MRADI WA RESOLVE (NbS) HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO

    October 03, 2025
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.