• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Hifadhi ya Milawilila

FURSA ZA UTALII KATIKA MSITU WA HIFADHI WA MILAWILILA

Mahali ulipoMsitu wa hifadhi wa Milawilila unapatikana kijiji cha Milawilila kata ya TawaTarafa ya Matombo umbali wa kilomita 13 toka barabara kuu ya Bigwa –Kisaki(kupitia Matombo Msalabani). Msitu huu unasimamiwa na vijiji viwili ambavyo niMilawilila na Mifulu kilichopo kata ya Tegetero.Asili ya jina la msitu: Jina la msitu Milawilila limetokana na mti uitwao“Mlawilila” ambao haupatikani sehemu nyingine duniani. Sehemu kubwa yamsitu wa hifadhi imetawaliwa na miti hiyo.

Kibao elekezi cha kuonesha msitu wa hifadhi wa Milawilila


Wakazi wa kijiji cha Milawilila ni wakulima na wafugaji. Mazao yanayolimwakwa wingi ni ndizi, mananasi, machungwa na machenza kwa ajili yabiashara. Aidha wanakijiji wengi wamehamasika kupanda miti ya mbao aina yaMisederea kwa ajili ya ujenzi. Msitu wa Milawilila unafikika kwa urahisi kwanjia ya barabara.



Barabara ya kuelekea msitu wa hifadhi na Utalii wa kilimo(Agrotourism)

Shughuli za utalii katika vijiji vinavyozunguka msitu wa kijiji cha Milawilila 

Utalii wa mazao ya viungo: 

Mazao ya viungo kama iliki, pilipili manga,Mdalasini, karafuu na tangawizi ni moja ya mazao ya biashara yanayostawi vizuri katika eneo hili. Aidha, wageni wanapata fursa ya kufahamu mimea halisi inayozalisha viungo, mfano miti ya mdalasini, pilipili manga, iliki, karafuu namingineyo.

Miti ya karafuu pamoja na karafuu iliyovunwa (Utalii kilimo) ikiwa inakaushwa kwamaandalizi ya kupelekwa sokoni.


Miti inayopatikana ndani ya msitu

Ipo miti ya asili ikiwemo misufipori,Milengolengo, Mivule, Mikalati, mikangazi pamoja na mitiki ambayoimepandwa mipakani. Miti aina ya mianzi (bamboo forest) yenye tabia yakutunza vyanzo vya maji inapatikana katika msitu huu.

Msitu wa Mianzi (Bamboo forest) unaohifadhi vyanzo vya maji Wanyama wanaopatikana msituni: Wapo Mbega weusi na weupe, tumbili,kima, vyura na nyoka wa aina mbalimbali.

Wanyama katika hifadhi ya msitu wa Milawilila

Matumizi ya msitu: 

Kwa sehemu kubwa msitu unatumika kwa shughuli zakimila (matambiko) na hivyo kulindwa na wazee wa mila. Hali hii inafanya msitu ubaki katika hali ya uasilia ukilinda mimea na vyanzo vya maji kamaunavyoonekana katika picha.


Moja ya vyanzo vya maji katika msitu wa hifadhi Milawilila

Matumizi mengine ni tafiti za baioanuai kwa kupitia wataalamu toka vyuo vikuu.Wageni wanaotembelea msitu: 

Msitu huu ni kivutio kikubwa kwa wasanii/waigizaji wanaopiga picha katika maeneo ya hifadhi asilia. Wageni wengine niwatafiti ambao mara nyingi wanapitia kijiji jirani cha Mifulu kilichopo kata yaTegetero kwa ajili ya kukamilisha taratibu za kuingia msituni.Muda wa kutembelea msituni: Muda mzuri wa kutembelea msituni ni kuanzia mwezi Mei hadi Septemba kwa vile kuanzia mwezi Oktoba hadi Aprili nimsimu wa mvua za vuli pamoja na masika.Shughuli za utalii zinazoweza kufanyika: Kuongoza wageni kupitia njia za miguu, kuona dawa za asili ndani ya msitu, kuona matunda yaasili,kutembelea maeneo ya matambiko, kusikiliza sauti za ndege nawanyama.


Safari za miguu ndani ya msitu wa hifadhi- Milawilila

Eneo la kuweka kambi (camping sites): Ndani ya msitu wa hifadhi yapomaeneo yaliyotengwa kwa ajili ya kuweka kambi (camp sites) kwa wageni wanaohitaji kupumzika.

Daraja la zege Mto Mvuha Daraja hili ni mpaka kati ya kijiji cha Milawilila na kijiji cha Mifulu kilichopo kataya Tegetero. Katika eneo hili watalii wanapata fursa ya kuona mipaka baina ya vijiji viwili. Daraja hili limerahisisha huduma ya mawasiliano baina ya vijiji viwili vinavyopakana na msitu.


Daraja linalotenganisha kijiji cha Milawilila (Tawa) na kjijicha Mifulu (Tegetero)


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 10, 2025
  • TANGAZO A UPANGA VYUMBA VYA OFISI NA MAENEO MBALIMBALI YALIYOPO MOROGORO MJINI March 19, 2025
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • ORODHA YA WANAFUNZI WA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO AWAMU YA PILI 2018. September 07, 2018
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI: MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 12, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEEA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO,MAAGIZO YATOLEWA

    April 11, 2025
  • KATIBU TAWALA MKOA WA MOROGORO AENDELEZA KAMPENI YA JISOMESHE NA MKARAFU

    March 14, 2025
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.