• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

NAIBU WAZIRI OR-TAMISEMI (AFYA) AAGIZA UKAMILISHWAJI WA WODI 3 HADI KUFIKIA JULAI 19, 2021.

Imetolewa: June 19th, 2021

Naibu Waziri OR-TAMISEMI (Afya) Mhe. Dkt. Festo John Dugange amefanya Ziara ya siku moja kukagua miradi ya afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro ambapo awali alikuwa atembelee Zahanati ya Kibuko ambayo ilianzishwa kwa nguvu za wananchi lakini pia Hospitali ya Wilaya inayoendelea kujengwa (Mvuha), lakini Mhe. Naibu Waziri alifanikiwa kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya Juni 19, 2021.

Naibu Waziri OR-TAMISEMI (Afya) Mhe. Dkt. Festo J. Dugange ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro kumaliza ujenzi wa Wodi 3 za watoto, wanawake na wanaume ifikapo Julai 19, 2021 kama ambavyo Mhandisi wa Halmashauri ameeleza kwamba ifikapo Julai 19 majengo hayo yatakuwa yamekamilika.

"Tumegundua kwamba mmechelewa kukamilisha miradi kwa Kadri ya maelekezo ya Serikali na mumetoa maelezo yenu lakini moja tu zuri ambalo mumeniahidi ni kwamba ifikapo tarehe 19 ya mwezi wa saba kwamba majengo haya yote yatakuwa yamekamilika. Na mimi nawaelekeza muhakikishe usiku na mchana mnapambana kwa kuzingatia ubora, viwango na thamani ya fedha Wodi hizi zikamilike kama ambavyo mumesema wenyewe."

Katika hatua nyingine Mhe. Dkt. Festo J. Dugange amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro kwa usimamizi mzuri wa miradi ya afya licha ya kuwa na watumishi wachache hasa kwenye idara ya ujenzi.

"Niwapongeze sana kwa maana ya ubora wa majengo kwa kweli ubora wa majengo unaona kabisa yana thamani ya fedha ambayo mpaka sasa imeshatumika, mumejenga kwa kuzingatia viwango na unadhifu mzuri lakini usimamizi mzuri pamoja ni kwamba kuna engineer (Mhandisi) mmoja tu na miradi ni mingi sana lakini kwa kweli Mkurugenzi hongera sana mumejitahidi sana kama Halmashauri kusimamia hii miradi."

Aidha akisoma taarifa ya idara ya afya ya Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, Mkurugenzi Mtendaji Bi. Rehema S. Bwasi amesema, "Kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2018/2019 hadi sasa tumepokea fedha kutoka Serikali kuu kiasi cha Shilingi Bilioni tano na Milioni Mia moja na hamsini kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya 6, Hospitali ya Wilaya pamoja na Zahanati 7"

Lakini pia kwenye taarifa hiyo Bi. Rehema S. Bwasi ametoa taarifa ya kupungua kwa vifo vya mama wajawazito na watoto wachanga toka 2018 hadi sasa.

Akiongea na timu hiyo ya wakuu wa idara na vitengo ya Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, Mhe. Dkt. Festo Dugange amesema, "Mmeendelea kwa kiasi kikubwa sana kupunguza kasi ya vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga, nikiangalia mmetaja kwa miaka mfululizo 2018, 2019, 2020 tunaona kabisa ile trend ni ya kushuka chini. Kwa hiyo niwapongeze sana Dkt. Manyerere na timu yako ya CHMT"

Aidha Mhe. Dkt. Festo Dugange amezungumzia kuhusu CHF iliyoboreshwa na kusema, "Jambo kubwa katika CHF ni Uhamasishaji na ili uhamasishe vizuri kwenye CHF ni lazima Dawa zipatikane ili wale uliowasajiri awamu ya Kwanza wakawe mabalozi wazuri kuwasemea kwa jamii kwamba CHF inafaa."

Katika hatua nyingine Mhe. Dkt. Festo Dugange amewaambia timu hiyo ya wakuu wa idara na vitengo kwamba Serikali inatambua na kuthamini kazi wanayoifanya katika kuhudumia Wananchi.

#KAZI IENDELEE

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO A UPANGA VYUMBA VYA OFISI NA MAENEO MBALIMBALI YALIYOPO MOROGORO MJINI March 19, 2025
  • TANGAZO LA KAZI YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU, DEREVA NA MTENDAJI WA KIJIJI July 15, 2024
  • TANGAZO LA RASIMU July 25, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI: MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 12, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEEA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO,MAAGIZO YATOLEWA

    April 11, 2025
  • KATIBU TAWALA MKOA WA MOROGORO AENDELEZA KAMPENI YA JISOMESHE NA MKARAFU

    March 14, 2025
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.