MAENEO YA MILA NA DESTURI, HISTORIA NA KIUTAMADUNI HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO
S
|
JINA
|
ENEO
|
HISTORIA
|
1.
|
MWAMBA WA FUKWE |
TEGETERO |
Mwamba huu uko umbali wa km 57 kutoka Morogoro mjini. Eneo hili hufikika kwa wastani wa masaa mawili kutokea Kanisa la Tegetero.
Mwamba huu umezungukwa na msitu wa asili wa Ugulo katika eneo la Tegetero,ni miongoni mwa maeneo yanayovutiwa na watalii una mandhali ya kuvutia kwa kupumzikia na kuweka kambi ili kuangalia maeneo ya milima na maporomoko ya maji kwa upande wa Kaskazini wa Mwamba huo. Katika Mwamba huu kuna kambi tatu zilizopo katika msitu wa eneo la Fukwe hutumiwa na watalii kutembelea na kuangalia ndege na maua aina ya “Saint Pauline”. Katika msitu wa Ugulo kuna ndege waitwao “Uluguru Bush light”wenye maumbo makubwa rangi nyekundu na nyeusi ambao hpendelea kuishi katika miti mikubwa ya Msitu huo mnene. |
2.
|
KIJIJI CHA KIMILA
|
KINOLE
|
Kijiji cha Kinole kiko eneo la pembezoni mwa mji wa Morogoro umbali wa km 45 kutoka Morogoro mjini .
Ukifika Kijiji cha Kinole unaweza kufanya yafuatayo,
|
3
|
MWAMBA WA MATOMBO NA MAPANGO YA MATOMBO
|
MATOMBO
|
Katika Miamba ya Matombo kuna mawe yalioshikana mithiri ya Matiti ya Mwanamke hujulikana kwa jina la Matombo.
Neno matombo asili yake matiti ya Mwanamke kwa lugha ya Kiluguru. Mapango haya yanafikika kwa urahisi yana mandhali nzuri na sehemu nadhifu ya kupumzikia kwa ndani. Wakazi wa eneo hilo hutumia mapango haya kwa shughuli za kimila. |
4.
|
MILIMA YA KOLELO
|
KOLELO
|
Jina la mzimu maarufu sana Morogoro ,Asili ya jina la mwanamke Ajuza Bibi aliyepewa karamu na mwenyezimungu ya kutibu na kutatua matatizo ya watu mbalimbali huko mlima Kolelo kwenye Pango ambalo mzimu wake ulifanya maajabu.
Alipofariki mzimu wake uliendelea kuwachagua watoto wa kurithi mikoba. Kaburi la bibi huyu lipo mpaka leo huko Lubasazi (Kolelo) ukitaka kufika waone walinzi wa milima Kolelo. Zipo simulizi Lukuki kwa miujiza ya Kolelo na Mlima wenyewe .Kubwa ni ile ya ufumbuzi wa matatizo ya kijamii, mfano magonjwa, kukosa mtoto kwa muda mrefu. Hii ni sehemu maarufu kwa shughuli za Kimila kama matambiko ambayo hufanyika kipindi cha Mwezi Disemba kwa kila Mwaka . Katika mapango ya misitu ya Kolelo watalii wanaweza kufika na kujionea desturi na Tamaduni za Makabila ya Kiluguru na wakutu pindi wanapofanya maombi kwa mizimu |
5.
|
MAPOROMOKO YA MAJI MLULU
|
MTOMBOZI
|
Maporomoko ya maji ya Mlulu yapo katika Kata ya Mtombozi ni kivutio kikubwa cha Utalii.
Maporomoko hayo yanapatikana umbali wa km 85 kutoka Morogoro Mjini na yanafikika kwa urahisi nyakati zote. utafiti uliofanywa na Shirika la Umeme TANESCO umeeleza kuwa maporomoko haya yanaweza kuzalisha umeme wa kilowati 2. |
6.
|
MSITU WA KIMBOZA ( BWAWA LA KIMBOZA CHOKA WAHAWI PANGO LA NJIWA MBEGA WEUSI VIPEPEO MIJUSI –GECKO VINYONGA)
|
KIBUKO
|
Msitu wa Kimboza ni miongozi mwa mali kale zinazotumika kuhifadhi historia na utamadui wa makabila Nchini.
Msitu huu una ukubwa wa Hekta 405 na upo umbali wa km 51 kutoka Morogoro barabara ya Matombo kuelekea Kisaki na umepakana na vijiji vinne vilivyopo katika Tarafa ya Mkuyuni pamoja na Matombo. Msitu huo una miti mingi inayotumiwa kwa ajili ya dawa za asili muhimu kwa kutunza vipepeo wenye rangi mbalimbali vya kuvutia, vinyonga wadogo na mijusi ambayo imeelezwa haipatikani sehemu nyingine duniani. Msitu wa Kimboza wanapatikana wanyama aina ya Mbegu na ndege wa kila aina wakiwemo njiwapori kabla ya mwaka 1922 Kwenye msitu kuna Mwamba wa jiwe ambao inaelezwa lilitumika ,kutolea adhabu kali kwa wachawi. Kwa mujibu wa taarifa za wazawa karne ya 19 msitu huu ulitumiwa na machifu wa kabila la waluguru kama eneo maalumu la kutolea adhabu ya kuwachoma moto watu waliokuwa wamethibitika ni wachawi. Simulizi za kale zinasema watu wote ambao walibainika kuwa ni wachawi walipelekwa kwenye pango lenye jiwe maalumu kwa ajili ya kuwachoma ambapo hufungwa kamba mikono na miguu halafu anaingizwa ndani ya jiwe . Machifu wa Kiluguru walitenga eneo hilo maalumu na kuliita “Choka wahawi” . Adhabu hizo ziliisha baada yaTanganyika kupata Uhuru wake mwaka 1961. Simulizi zinaeleza kwenye msitu huu kuna sehemu ya makumbusho ya kihistoria ya Kijadi ya Kabila la Waluguru ambapo pia ndani ya Msitu huo kuna maeneo yamepewa majina ya “Dago la Njiwa”ambalo wanajumuika njiwa pori ambao wanaoga kwa kutumia majivu . |
7.
|
USOLO
|
MVUHA (TAMBUU)
|
Eneo hili liliwahi kutumiwa na viongozi wa jamii ya Kabila la Waluguru ,Chifu Kingalu wa kwanza na Hega kwa kile wanachosadikiwa kuonyesha umahili wao wa kuchonga juu ya sakafu ya Miamba ya Mawe kwa Kisigino karne kadhaa zilizopita huko kijiji cha Tambuu
Taarifa zimebainisha kuwa viongozi hao wa jadi walikuwa na ushindani wa kimadaraka na kupelekea kukutana katika makutano ya Mito ya Mtombozi na mngazi na kuunda Mto-Mvuha. Kiongozi wa jadi chifu Kingalu wa kwanza na Hega waliwahi kushindana nani mwenye uwezo na nguvu za kiutawala jamii inayoishi milima ya uluguru ambapo katika ushindani huo walilazimika kuoneshana umwamba wa kuchonga mwamba wa jiwe kwa kutumia visigino (Usolo /mchezo wa Bao) Ukifika katika makutano ya Mto Mtombozi na mngazi na kuunda mto mvuha katika Mwamba wa jiwe uliochongwa katika kutumia ncha ya Kisigino. Kitongoji cha Usolo kiko katika kijiji cha Tambuu na kushuhudia vishimo vilivyosadikiwa kuchimbwa kwa kutumia ncha ya visigino vya viongozi wa jadi chief Kingalu na Chief Hega katika ushindani wao. Taarifa zinasema Kingalu aliweza kumzidi mwenzake maarifa kwa kuchimba vishimo 36 huku Hega akiambulia vishimo 16 pekee ambapo baada ya ushindani huo waliweka mipaka ya kiutawala Hega aliweza kumiliki eneo la ardhi kuelekea Kisaki ambapo Kingalu aliendelea kutawala eneo la Kinole hadi leo,utawala wa sasa wa jamii ya waluguru ni wa chief Kingalu Mwanabanzi 15 ambaye anaishi katika kijiji cha kinole huku mila na desturi zikiendelea kuanziwa kwa kufanya Tambiko kila mwaka kwa kuomba ustawi wa jamii. |
8.
|
CHIEF KINGALU 15
|
KINOLE
|
Chief Kingalu Mwanabanzi wa 15 Mtawala wa waluguru wa Matombo.
Miaka 300 iliyopita waluguru waliingia katika milima ya Uluguru wakiongozwa na machifu watatu wakuu. i.Chief Mbagho wa Waluguru wa Mgeta ambaye alipiga Kambi yake vidighisi. ii.Chief Kingalu ambaye baadaye kwa namna ya ajabu mzimu wake yulisafiri hadi Turiani ambako Matambiko yanafanyika. iii.Hegga wa Waluguru wa Kisaki Chief Kingalu mwanabanzi anafuata mstari wa Kingalu aliitisha waluguru wenye koo zinazoheshimu utawala huo hasa katika utamaduni wa Matambiko. iv.Chief Mbagho aliona ujio wa wajerumani na waarabu ndiye aliyetabiri kuwapo kwa kijana mdogo ambaye atawaondoa wageni katika Tanganyika simulizi zinasadiki kijana huyo ni Mwalimu Nyerere. |
9.
|
MZIMU WA WALUGURU
|
KOLELO
|
Eneo hili la Kolelo kwa miaka nenda miaka rudi ni alama moja muhimu ya temi takribani tatu zinazofanya kabila la waluguru.
Kolelo ni mzimu ni jina la mahali na alama katika mambo mengi na makubwa ya kihistoria yaliyotokea Uluguru. Temi zinazotumia ni zile zilizoongezwa na Hegga ,Mbagho na Kingwalu. simulizi zinasema kulikuwa na wanawake wawili ndugu waliokwenda kusenya kuni msituni.Bila shaka karibu na mlima Kolelo mmoja akapotea inasadikiwa alibebwa na joka hadi pangoni wakamtafuta wakakata tama. Baada ya muda akatokea akiwa na mkoba wa uganga .Mkoba huo alivyorudi nao kutoka Pango la Kolelo ndio uliotumika kuikomboa jamii dhidi ya madhila mboka huu ukaarithiwa kutoka kizazi hazi kizazi. Kolelo ni mahali pasafi wachafu hawafiki huko ama sivyo wataumbika hasa uchafu wa Matendo na Tabia ujumbe wa Kolelo ni kuwataka watu wawe na matendo masafi na kurudia mila na Desturi. |
10.
|
CHEMCHEM YA MAJI
|
KISAKI
|
Uwepo chemchem ya maji moto Eneo linapatikana magharibi mwa Kisaki umbali wa kutoka Stesheni km 5,chemchem hii ni kivutio kikubwaa cha utalii na shughuli za kimila hufanyika kwenye eneo hilo ikiwemo matambiko , hata hivho maji hayo hutumika kama dawa ya ngozi.
|
11.
|
BWAWA LA VIBOKO
|
LUKULUNGE
|
Bwawa hili lina viboko wengi ambapo wageni mbalimbali hufika kwa ajili ya kujionea viboko walioko kwenye Bwawa hili .
Shughuli za uvuvi hufanyika na kuwapatia wananchi chakula na kujikwamua kiuchumi hasa wavuvi. |
Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road
Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania
Simu: +255 23 2935458
Simu ya Kiganjani:
Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz
Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.