• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MWENGE WA UHURU WAPOKELEEA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO,MAAGIZO YATOLEWA

Imetolewa: April 11th, 2025

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA 2025 ATOA MAAGIZO.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2025, Bw. Ismail Ali Ussi, ameutaka uongozi wa Wilaya ya Morogoro kuhakikisha unatatua changamoto zilizopo katika soko la chakula la Ngerengere ili wananchi wa Ngerengere na wengine wanaolitumia soko hilo waweze kufanya biashara zao ndani ya soko hilo bila bughudha yoyote.



Bw. Ussi ametoa agizo hilo Aprili 11, 2025, wakati akikagua soko hilo ikiwa ni siku ya kwanza ya Mbio za Mwenge wa Uhuru kuwasili Mkoani Morogoro kwa ajili ya kuzindua, kuweka mawe ya msingi na kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani humo.



Amesema kuna umuhimu mkubwa kwa Mkuu wa Wilaya hiyo, Mhe. Mussa Kilakala, pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro kushughulikia changamoto zote zinazolikabili soko hilo, zikiwemo miundombinu ya maji na vyoo, ili wafanyabiashara waweze kufanya kazi zao pasipo shida kwa maendeleo yao binafsi na ya taifa kwa ujumla.


“Kuna baadhi ya changamoto ambazo nimeziona katika soko hili; kabla hatujafika mkoa wa tano, marekebisho yafanyike na tupate taarifa,” amesema Bw. Ussi.


Aidha, amewataka wananchi wa Tarafa ya Ngerengere kutunza miundombinu iliyopo ndani ya soko hilo na kuitumia ipasavyo ili iweze kudumu kwa muda mrefu, kwani serikali hutumia fedha nyingi kuijenga.


Katika hatua nyingine, Bw. Ussi amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inalenga kuboresha maisha ya Watanzania katika sekta mbalimbali, ikiwemo sekta ya afya na upatikanaji wa maji vijijini.


Pia, ameishukuru jamii ya Kata ya Mikese kwa kuwakaribisha wawekezaji, hususan mwekezaji wa mradi wa ujenzi wa kiwanda cha kutengeneza nguzo za umeme za zege kitakachogharimu zaidi ya shilingi bilioni 3.5 hadi kukamilika kwake, na ambacho kinatarajiwa kutoa ajira kwa wananchi wapatao 120 wa tarafa hiyo.


Ameongeza kuwa kiwanda hicho kitasaidia kupunguza changamoto ya nguzo zinazodondoka, hali inayosababisha kukatika kwa umeme mara kwa mara, na kuwataka wananchi kukitunza kiwanda hicho kwa manufaa yao na vizazi vijavyo.


Mbio za Mwenge wa Uhuru mkoani Morogoro, katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, zimetembelea jumla ya miradi nane yenye thamani ya shilingi bilioni 4.4. Mwisho wa mbio hizo ulihudhuriwa na Bw. Ussi ambaye alifunga kongamano la vijana lililofanyika kwa siku saba na kujikita katika mafunzo ya uzalendo, maadili mema, na ujasiriamali.



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO A UPANGA VYUMBA VYA OFISI NA MAENEO MBALIMBALI YALIYOPO MOROGORO MJINI March 19, 2025
  • TANGAZO LA KAZI YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU, DEREVA NA MTENDAJI WA KIJIJI July 15, 2024
  • TANGAZO LA RASIMU July 25, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 12, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEEA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO,MAAGIZO YATOLEWA

    April 11, 2025
  • KATIBU TAWALA MKOA WA MOROGORO AENDELEZA KAMPENI YA JISOMESHE NA MKARAFU

    March 14, 2025
  • "BAINISHENI VYANZO VYA MAJI NA MVILINDE" MHE.KASSIM MAJALIWA MAJALIWA

    March 05, 2025
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.