• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

.

Imetolewa: October 7th, 2018

Serikali imesema kuwa  mwaka wa fedha 2017/2018 jumla ya Sh bilioni 553.39 zimekusanywa kati ya Sh bilioni 687.31 ambazo ni sawa na asilimia 81 ya lengo ambalo halmashauri zote nchini ilijiwekea.

Aidha, Dodoma imeongoza katika ukusanyaji wa mapato kwa upande wa majiji na mikoa ambapo Halmashauri ya Mji Geita ikiwa kinara katika mlinganisho wa kiasilimia kwa Mamlaka zote za Serikali za Mitaa bila ya kujali hadhi huku halmashauri ya Mbinga ikishika mkia.

Akitangaza makusanyo kwa halmashauri zilizofanya vizuri na vibaya, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo alisema: " TAMISEMI imekuwa ikifuatilia ukusanyaji wa mapato katika halmashauri zake ili kuweza kufanikisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika halmashauri zote nchini.

" Baada ya kumaliza zoezi la usuluhishi wa kibenki takwimu zinaonyesha kwamba kwa mwaka wa fedha 2017/2018 jumla ya shilingi 553,390,075,912 zimekusanywa kati ya shilingi 687,306,661,000 ambazo ni sawa na asilimia 81 ya lengo."

Jafo alisema kwa upande wa Majiji, Jiji la Dodoma limekuwa la kwanza kati ya majiji sita likiwa limekusanya Sh bilioni 25.06 kati ya Sh bilioni 19.33 ambayo ni sawa na asilimia 130 ya lengo wakati Jiji la Mbeya limekuwa la mwisho kwa kukusanya kiasi cha Sh bilioni 7.82 kati ya Sh bilioni 11.0, sawa na asilimia 71.

Dar es Salaam ni ya pili ikiwa imekusanya Sh bilioni 15.67 kati ya makisio ya Sh bilioni 16.41 ambayo ni asilimia 95, Arusha ya tatu ikikusanya Sh bilioni 13.59 kati ya lengo la Sh bilioni 14.58, Mwanza imeshika nafasi ya nne ikikusanya Sh bilioni 10.47 kati ya malengo ya Sh bilioni 1.44, Tanga ikikusanya Sh bilioni 10.84 kati ya malengo ya Sh bilioni 14.03.

Jafo alisema Manispaa ya Iringa ndiyo ilikuwa ya kwanza kwa kukusanya Sh bilioni 4.28  kati ya Sh 4.17 ambayo sawa na asilimia 103 ikifuatiwa na Manispaa ya Temeke iliyokusanya Sh bilioni 29.41 kati ya lengo la kukusanya Sh bilioni 29.07 sawa na asilimia 101.

Alisema katika kundi hili, Manispaa ya Ilemela ilikuwa ya mwisho kwa kukusanya Sh bilioni 4.76  kati ya lengo la kukusanya Sh bilioni 11.75 sawa na asilimia 40.

Jafo alisema Halmashauri ya Mji wa Geita ndiyo ilikuwa ya kwanza kwa kukusanya Sh bilioni 6.86 kati ya lengo la kukusanya Sh bilioni 3.15 sawa na asilimia 218 ikifuatiwa na Halmashauri ya Mji wa Njombe iliyokusanya Sh bilioni  2.93 kati ya lengo la kukusanya Sh bilioni 2.40 sawa na asilimia 122.

Alisema Halmashauri ya Mji wa Nanyamba ni ya mwisho kwa kukusanya Sh bilioni 1.14 kati ya lengo la kukusanya Sh bilioni 2.11 sawa na asilimia 54.

Jafo alisema Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha ilikuwa kinara kwa kukusanya Sh bilioni 3.09 kati ya Sh bilioni 1.87 sawa na asilimia 165 ikifuatiwa na Halmashauri ya Mpimbwe iliyokusanya Sh bilioni 1. 55 kati ya Sh milioni 956.84 sawa na asilimia 162.

Alisema halmashauri za wilaya zilizofanya vibaya zaidi ni pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga iliyokusanya asilimia 20, halmashauri ya Songea iliyokusanya asilimia 33, Halmashauri ya Rorya ilikusanya asilimia 37 na Halmashauri ya Siha iliyokusanya asilimia 39.

Aidha, Jafo alisema katika mlinganisho wa kiasilimia kwa Mamlaka zote za Serikali za Mitaa bila ya kujali hadhi zao, halmashauri tatu kinara kwa makusanyo kiasilimia ni Halmashauri ya Mji wa Geita ambayo imekusanya kwa asilimia 218, Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha ambayo imekusanya kwa asilimia 165 na Halmashauri ya Mpimbwe iliyokusanya kwa asilimia 162 .

Bonyeza link kupata mchanganuo wa Hali ya Makusanyo Mamlaka za Serikali za Mitaa kiundani zaidi 

ASILIMIA YA MAKUSANYO YA MAPATO NDANI YA HALMASHAURI KWA MWAKA 2017-18.pdf

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 10, 2025
  • TANGAZO A UPANGA VYUMBA VYA OFISI NA MAENEO MBALIMBALI YALIYOPO MOROGORO MJINI March 19, 2025
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • ORODHA YA WANAFUNZI WA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO AWAMU YA PILI 2018. September 07, 2018
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI: MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 12, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEEA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO,MAAGIZO YATOLEWA

    April 11, 2025
  • KATIBU TAWALA MKOA WA MOROGORO AENDELEZA KAMPENI YA JISOMESHE NA MKARAFU

    March 14, 2025
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.