• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

.

Imetolewa: May 2nd, 2021

Na Tajiri Kihemba.

Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro, Mhandisi Emmanuel Kalobelo ambae ni Mgeni rasmi katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani kimkoa yaliyofanyika katika uwanja wa  Jamhuri Morogoro amekabidhi vyeti kwa wafanyakazi hodari toka Taasisi mbalimbali zilizopo ndani ya Mkoa wa Morogoro na kuhutubia hadhara ya Wafanyakazi na Wananchi waliofika uwanjani hapo.

Katika hotuba yake Mhandisi Emmanuel Kalobelo amesema, "Waajiri waweke mazingira wezeshi ya kuwepo kwa vyama vya Wafanyakazi na kuacha tabia ya kudhohofisha vyama vya Wafanyakazi na haki za Wafanyakazi kwani hiyo sio dhamira ya Serikali yetu, uzoefu unaonyesha kuwa pale ambapo kuna matawi ya vyama vya Wafanyakazi ambayo yanatimiza majukumu yake vizuri na menejimenti inatimiza wajibu wake ipasavyo, uhusiano wa kikazi huwa mzuri"

Mhandisi Emmanuel Kalobelo ameeleza zaidi kwa kusema, "hii husaidia kupunguza migogoro, kuepusha migomo na huongeza tija na ufanisi, matawi haya hutoa fursa ya majadiliano na mazungumzo Kati ya Wafanyakazi na waajiri, Uhuru wa Wafanyakazi kujiunga na vyama vya Wafanyakazi ipo kisheria na halina mjadala."

Katika hatua nyingine Mhandisi Emmanuel Kalobelo amesisitiza kuwa anaamini waajiri wa Mkoa wa Morogoro wengi ni wastaarabu na wanafuata Sheria, wale wachache wanaokiuka Sheria kwa makusudi wote anaomba apatiwe orodha ili aweze kufuatilia na kuhakikisha kwamba Sheria hiyo inasimamiwa na inafanya Kazi katika maeneo hayo.

Aidha akizungumzia swala la migogoro sehemu za kazi, Mhandisi Emmanuel Kalobelo amesema, "utatuzi wa migogoro ya kikazi kama mlivyozungumzia kwenye risala yenu, Serikali itawasiliana na wadau husika kwenye Wizara ili kuona uwezekano wa kufungua Ofisi ya idara ya Kazi kwenye maeneo yenye Wafanyakazi wengi katika Mkoa wetu wa Morogoro ili Wafanyakazi waweze kupata huduma hiyo kwa ukaribu."

Kuhusu ucheleweshwaji wa kesi za Wafanyakazi Mhandisi Kalobelo amesema, "Serikali itaendelea kuwawezesha majaji wa Mahakama kuu mara kwa mara kuamua kesi hizo, sambamba na hilo Serikali ipo hatua za mwisho kufungua Ofisi ya jaji mfawidhi wa Mahakama kuu kanda ya Morogoro."

Mhandisi Emmanuel Kalobelo pia ameiagiza Ofisi ya Afisa Kazi Mkoa wa Morogoro ihakikishe kaguzi za mara kwa mara kwenye maeneo ya Kazi zinafanyika ili kujiridhisha kama mikataba ya Wafanyakazi inazingatia sheria.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 10, 2025
  • TANGAZO A UPANGA VYUMBA VYA OFISI NA MAENEO MBALIMBALI YALIYOPO MOROGORO MJINI March 19, 2025
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • ORODHA YA WANAFUNZI WA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO AWAMU YA PILI 2018. September 07, 2018
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • SHILINGI MILIONI 538 NA LAKI NNE KUNUFAISHA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WALEMAVU

    June 20, 2025
  • MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI: MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 12, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEEA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO,MAAGIZO YATOLEWA

    April 11, 2025
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.