• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DC MSANDO ATOA MAAGIZO.

Imetolewa: November 11th, 2021

Na. Tajiri Kihemba, MOROGORO DC.

Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mhe Albert Msando leo Septemba 11, 2021 ameshiliki kikao cha Baraza la Madiwani kupitia taarifa za Kata kwa robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2021/2022 katika Ukumbi wa Mikutano Pangawe, Morogoro.

Akitoa nasaha zake Mkuu wa Wilaya, Mhe Albert Msando amewataka Maafisa Watendaji wa Kata, Waheshimiwa Madiwani na Wakuu wa Idara kusimamia ipasavyo ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri, utunzaji wa vyanzo vya maji na kusimamia Elimu na miundombinu yote ya elimu.

"Anaesimamia mapato yanayotokana na Kijiji husika ni Afisa Mtendaji wa Kijiji na kupeleka taarifa kwenye Kata hadi Halmashauri ya Wilaya, nawaagiza Maafisa Watendaji wa Kata taarifa zenu za Mapato zionekane kwenye taarifa hizi za robo." Amesema Mhe. Albert Msando.

Mhe. Albert Msando ameongeza kwa kusema kuwa kila mkuu wa Idara ana wajibu wa kukusanya mapato ya Halmashauri,

"Dt (Mwekahazina wa Halmashauri) sio Mkusanya mapato ni msimamizi wa mapato, Afisa Kilimo unatakiwa kuhakikisha mapato yatokanayo na Kilimo yanapatikana, Mwanasheria unahusika na faini zote za uvunjwaji wa Sheria  kwenye mapato." Amesema Mhe. Albert Msando.

Kwa upande wa Elimu Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe Albert Msando amesema kuwa pamoja na kusimamia ujenzi wa madarasa bado Maafisa Watendaji na Madiwani wakasimamie vizuri ukatili wa kijinsia kwa wanafunzi kwenye Kata zao ikiwa pamoja na kuzuia mimba zilizokithiri kwa watoto.

Mwisho Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe Albert Msando amesema Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Morogoro itaendelea kutoa ushirikiano kwa Maafisa Watendaji, Wakuu wa Idara na Waheshimiwa Madiwani ili kuweza kutekeleza majukumu vizuri.

#Barazalamadiwanikupitiataarifazakata

#morodcmpya

#tunatekelezakwakasiya5g

#Kaziiendelee

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO A UPANGA VYUMBA VYA OFISI NA MAENEO MBALIMBALI YALIYOPO MOROGORO MJINI March 19, 2025
  • TANGAZO LA KAZI YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU, DEREVA NA MTENDAJI WA KIJIJI July 15, 2024
  • TANGAZO LA RASIMU July 25, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 12, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEEA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO,MAAGIZO YATOLEWA

    April 11, 2025
  • KATIBU TAWALA MKOA WA MOROGORO AENDELEZA KAMPENI YA JISOMESHE NA MKARAFU

    March 14, 2025
  • "BAINISHENI VYANZO VYA MAJI NA MVILINDE" MHE.KASSIM MAJALIWA MAJALIWA

    March 05, 2025
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.