• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

SERIKALI YALETA MFUMO WA KUKUSANYA TAARIFA ZA VIFO.

Imetolewa: April 5th, 2022

Na. Tajiri Kihemba, MOROGORO DC.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Afya imedhamiria kukusanya taarifa za vifo vinavyotokea katika jamii ili kurahisisha upangaji wa mipango mbalimbali ya kimaendeleo kwa kutumia takwimu halisi za vizazi na vifo.

Hayo yamejidhihirisha leo Aprili 5, 2022 kupitia Mkutano maalumu wa Uhamasishaji juu ya Ukusanyaji wa taarifa za vifo vinavyotokea katika jamii ulioandaliwa na wataalamu kutoka Wizara ya Afya na Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro wakihusisha Madiwani na Maafisa Watendaji wa Kata Kumi za Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro.

Akielezea lengo la Mkutano huo Afisa Takwimu kutoka Wizara ya Afya, Ndugu Gisbert Msigwa amesema lengo ni kuwajulisha viongozi wa Mikoa, Halmashauri, Kata, Mitaa na Vijiji juu ya kuanza kwa zoezi la kufanya mahojiano ya vifo vinavyotokea katika jamii, kuelezea faida za kukusanya taarifa za vifo pamoja na kuelezea masuala mbalimbali yanayohusiana na mahojiano ya vifo vinavyotokea katika jamii.

Akizungumza kwa niaba ya Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, Mhe. Robe Zongo Robe amesema anaishukuru Serikali ya Rais @samia_suluhu_hassan kwa juhudi za makusudi za kuleta maendeleo katika Nchi yetu na kuahidi kutoa ushirikiano katika kuelimisha na kuhamasisha Wananchi kutoa taarifa za vifo kwa Maafisa Watendaji wa Kata ili kuwezesha takwimu hizo kutumika katika mipango mbalimbali ya Serikali.

Aidha, Maafisa Watendaji wa Kata wamepewa mamlaka na RITA ya kutoa vibali maalumu vya mazishi katika maeneo yao na muda mchache ujao Maafisa Watendaji hao watapatiwa mafunzo ya mfumo, hivyo vifo vyote vitakuwa vikirekodiwa katika mfumo maalumu ili kurahisisha upatikanaji wa takwimu hizo muhimu.

#SerikaliYaAwamuYaSitaKazini #morodcmpya

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO YA KAZI YA MUDA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 HALMASHAURI YA MOROGORO July 27, 2022
  • TANGAZO LA KAZI ZA UFUNDI WA MAJENGO (LOCAL FUNDI) January 13, 2023
  • TANGAZO LA KAZI ZA UFUNDI WA MAJENGO (LOCAL FUNDI) January 13, 2023
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOITWA KWENYE USAILI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 16, 2022
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • .

    May 24, 2023
  • .

    May 24, 2023
  • .

    February 04, 2023
  • MKUU WA MKOA WA MOROGORO BI. FATMA MWASSA AWAAPISHA WAKUU WA WILAYA

    January 28, 2023
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, Mvuha - Magogoni Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.