• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

KAMPENI YA CHANJO YA POLIO YAZINDULIWA.

Imetolewa: May 18th, 2022

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, Bi. Rehema S. Bwasi leo Mei 18, 2022 amezindua kampeni na zoezi la utoaji chanjo ya Polio kwa watoto wa umri chini ya miaka mitano.

Uzinduzi huo umefanyika katika Zahanati ya Mvuha katika Kijiji cha Mvuha ambapo kampeni hii sasa imeanza rasmi kwa wataalamu wa Afya kupita nyumba kwa nyumba kutoa Chanjo hiyo kwa watoto wa umri huo wa chini ya miaka mitano ili kuwakinga dhidi ya Ugonjwa huu wa Polio unasababisha kupooza kwa viungo vya mwili.

Akizungumza na Wananchi waliofika kwenye uzinduzi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, Bi. Rehema S. Bwasi amewataka Wananchi kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe @samia_suluhu_hassan katika kujali afya za Wananchi wake ndio maana sasa ameleta chanjo hii ya Polio baada ya Ugonjwa huu kuonekana katika Nchi jirani zinazopakana na Nchi yetu Tanzania.

"Nawaomba tujitokeze kwa wingi ili watoto wetu wapate chanjo hii ili kuwakinga na ugonjwa huu wa Polio unaosababisha kupooza, Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan anawapenda sana wananchi wake na ndio maana ameweka juhudi kubwa kuboresha sekta ya afya na kwa Halmashauri yetu ya Morogoro tumepokea fedha nyingi kwa ajili ya kujenga Vituo vya Afya, Zahanati, wodi za wanawake na wanaume, jengo la huduma za dharura, jengo la upasuaji wanawake na wanaume bila kusahau nyumba za watumishi wa afya ili waweze kutoa huduma za Afya kwa uhakika." Amesema Bi. Rehema Bwasi.

Katika hatua nyingine, Mlezi wa Timu ya wilaya ya uendeshaji wa huduma za afya (CHMT) ya Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, Bi. Neema Shanalingigwa amewataka Wananchi hao kuipokea chanjo ya Polio na kuhakikisha watoto wote wanapata Chanjo hiyo.

Naye Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, Dkt. Robert Manyerere amesema Kampeni hii imeanza rasmi baada ya Mkurugenzi Mtendaji Bi. Rehema S. Bwasi kuzindua na itafanyika nyumba kwa nyumba watoto wote wafikiwe.

Kutokana na Nchi jirani kuripoti kuwepo kwa ugonjwa huu, Serikali ya Tanzania imeamua kutoa Chanjo ya Polio ili kuwakinga watoto wote.

#TuwakingeDhidiYaPolio #SENSA_AGOSTI23

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO A UPANGA VYUMBA VYA OFISI NA MAENEO MBALIMBALI YALIYOPO MOROGORO MJINI March 19, 2025
  • TANGAZO LA KAZI YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU, DEREVA NA MTENDAJI WA KIJIJI July 15, 2024
  • TANGAZO LA RASIMU July 25, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 12, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEEA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO,MAAGIZO YATOLEWA

    April 11, 2025
  • KATIBU TAWALA MKOA WA MOROGORO AENDELEZA KAMPENI YA JISOMESHE NA MKARAFU

    March 14, 2025
  • "BAINISHENI VYANZO VYA MAJI NA MVILINDE" MHE.KASSIM MAJALIWA MAJALIWA

    March 05, 2025
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.