• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

E-MAC WAJITAMBULISHA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO.

Imetolewa: January 30th, 2024

Shirika lisilo la Serikali la maendeleo E-MAC limetambulisha mradi wa 'FEED THE FUTURE TANZANIA IMARISHA SEKTA BINAFSI' katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro.Kikao Cha kutambulisha mradi huo kimefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya Morogoro ambapo mradi umetambulishwa kwa wataalamu na wakuu wa idara mbalimbali za Halmashauri ili kupata ushirikiano katika utekelezaji.

Akiongea kwa niaba ya shirika hilo, Msimamizi wa Mradi Bi. Naomi Lukumay ameeleza lengo la mradi  katika Halmashauri na baadhi ya maeneo kuwa ni kusaidia vijana wajasiriamali binafsi."Lengo la mradi huu ni kusaidia vijana waliopo kwenye sekta ya kilimo kutambua fursa na kuzitumia yaani 'access to and use of financial and market resources '...." alisema Bi. Naomi

Mradi huu wenye kauli mbiu Tanzania Imarisha Sekta Binafsi unalenga kuwajengea uwezo vijana wajasiriamali zaidi ya 200 wa sekta binafsi kuelewa upatikanaji na matumizi ya huduma za biashara na fedha pamoja na fursa zinazolingana na mahitaji, uwezo na matarajio yao.

Aidha Bi. Naomi ameeleza kuwa Mradi huu ni wa miaka mine, ulioanza utekelezaji wake mnamo mwezi Mei 2022 na unatarajia kuongeza uelewa wa vijana juu ya sera, sheria na miongozo ihusuyo uchumi wao pamoja na kufahamu umuhimu wa kusajili biashara zao, kupata ujuzi wa jinsi ya usindikaji wa mazao, kupata masoko ya uhakika ya bidhaa wanazozalisha, kuongeza mauzo pamoja na kuongeza ujuzi juu ya elimu ya kilimo endelevu na ushiriki kwenye mijadala ya sera.Bi. Naomi amefafanua kuwa, vijana watapaswa kuchangia asilimia 30 ya gharama ya vifaa wanavyovihitaji katika biashara zao na mradi utawafadhili kwa asilimia 70 ili waweze kufikia malengo yao katika kujiimarisha kiuchumi kupitia sekta binafsi kwa upande wa biashara na kilimo.

Nae Mratibu wa mradi Ndg. Samweli Luhaga ameshukuru kwa ushirikiano walioupata kutoka kwa uongozi wa Halmashauri na kuomba uendelezwe kwa manufaa ya vijana katika kuimarisha sekta binafsi haswa kwa vijana wajasiriamali kwa upande wa kilimo.

Bw. Chesco Lwaduka Kwa niaba ya Mkurugenzi  amelitaka shirika hilo kutimiza malengo na kusimamia kanuni na taratibu kipindi chote cha utekelezaji wa mradi.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 10, 2025
  • TANGAZO A UPANGA VYUMBA VYA OFISI NA MAENEO MBALIMBALI YALIYOPO MOROGORO MJINI March 19, 2025
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • ORODHA YA WANAFUNZI WA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO AWAMU YA PILI 2018. September 07, 2018
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • SHILINGI MILIONI 538 NA LAKI NNE KUNUFAISHA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WALEMAVU

    June 20, 2025
  • MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI: MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 12, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEEA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO,MAAGIZO YATOLEWA

    April 11, 2025
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.