• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

KAMATI YA BUNGE YA TAMISEMI KUKAGUA MIRADI YA SEQUIP, BOOST MOROGORO.

Imetolewa: February 19th, 2024

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa – TAMISEMI inatarajia kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo ya Sekta ya Elimu Mkoani Morogoro inayotekelezwa chini ya mradi wa kuimarisha elimu ya Sekondari – SEQUIP na kuimarisha elimu ya Awali na Msingi – BOOST katika Halmashauri Nne za Mkoa huo.



Hayo yamebainishwa Februari 19, 2024 na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima wakati akitoa taarifa ya miradi hiyo ambayo moja ya miradi itakayotembelewa ni Ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Morogoro iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro DC.

Akitoa taarifa ya miradi hiyo Mkuu wa Mkoa huo amegusia changamoto ya Mradi wa Sekondari ya Wasichana ya Morogoro huku akiiomba Kamati hiyo ya Bunge kutupia jicho la pekee mradi huo kutokana na changamoto kubwa iliyopo katika utekelezaji wake mradi ambao unagharimu jumla shilingi Bil. 3.



“...hili la shule ya sekondari ya bilioni tatu…kuna kamati ya usimamizi lakini ule muundo mzima wa kusimamia ile hela ni jambo la ajabu sijawahi kuona…” amesema Mkuu wa Mkoa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Dennis Londo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mikumi kwa niaba ya wajumbe wengine wa Kamati hiyo ameonesha dhamira yao ya kuitaka Serikali kudhibiti matumizi mabaya ya fedha zinazotokana na mapato ya Halmashauri kwa kuwa amesema fedha zinazotoka Serikali Kuu zinalemaza Halmashauri nyingi hapa nchini.



Aidha, Mwenyekiti huyo ameeleza kwa ufupi maazimio ya kamati hiyo ambayo yatajadiliwa kipindi cha Bajeti kuwa ni pamoja na masuala mtambuka kama suala la Lishe, taulo za kike, ukusanyaji na matumizi na mapato ya ndani, viwanja vya michezo na miundombinu ya shule kama vile vyoo, Madarasa na utoshelevu wa madawati.





Katika hatua nyingine, Mhe. Dennis Londo amempongeza Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Adam Kighoma Malima kwa ubunifu wake kwa kuzifanyia tathmini Halmashauri za Mkoa huo kwa lengo la kuboresha utendaji kazi wao na kuimarisha usimamizi wa fedha za Serikali wanazokusanya katika Halmashauri zao na zile zinazopokelewa kutoka Serikali Kuu.



Kwa mujibu wa Ratiba iliyotolewa, Kamati hiyo itatembelea Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, Mvomero, Kilosa, Ifakara na Halmashauri ya Mlimba kuanzia Februari 19 hadi Februari 24, 2024.


MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO A UPANGA VYUMBA VYA OFISI NA MAENEO MBALIMBALI YALIYOPO MOROGORO MJINI March 19, 2025
  • TANGAZO LA KAZI YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU, DEREVA NA MTENDAJI WA KIJIJI July 15, 2024
  • TANGAZO LA RASIMU July 25, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 12, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEEA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO,MAAGIZO YATOLEWA

    April 11, 2025
  • KATIBU TAWALA MKOA WA MOROGORO AENDELEZA KAMPENI YA JISOMESHE NA MKARAFU

    March 14, 2025
  • "BAINISHENI VYANZO VYA MAJI NA MVILINDE" MHE.KASSIM MAJALIWA MAJALIWA

    March 05, 2025
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.