• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

KAMATI YA FEDHA,UONGOZI NA MIPANGO YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO INAYOENDELEA KUTEKELEZWA.

Imetolewa: May 5th, 2021

TAJIRI KIHEMBA, Moro Dc

Kamati ya fedha,uongozi na mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro imefanya ziara yake ya kukagua miradi ikiwa ni ziara yake ya kukamilisha taarifa ya robo ya tatu kwa mwaka wa fedha wa 2020/2021.

Ziara hiyo imefanyika kwa siku mbili mfululizo kuanzia tarehe 3 Mei hadi 4 Mei mwaka 2021 ambapo wajumbe walipata fursa ya kutembelea ujenzi unaoendelea katika maeneo ya Shule ya Sekondari Mikese, Sekondari ya Nelson Mandela, Zahanati ya Mhunga Mkola, Sekondari ya Tomondo, Soko la Mkuyuni, Sekondari ya Matombo, Sekondari ya Mtombozi, Zahanati ya Lundi, Jengo la Utawala la Halmashauri (Mvuha) na Wodi za wanawake, wanaume na watoto katika Hospitali ya Wilaya.

Lakini pia Kamati ilipata fursa ya kukagua magari ya Halmashauri yanayoendelea na utengenezwaji katika karakana za Halmashauri na karakana nyingine TEMESA na TOYOTA ambapo Kamati kupitia Mwenyekiti wake ambae pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri, Mhe. Lucas J. Lemomo imewataka wadau hao wafanye tathmini zao za mwisho na wawasilishe taarifa ya ubovu wa magari na gharama za utengenezaji ili Halmashauri ione zile gari zinazoweza kutengenezwa kwa haraka ziweze kutengenezwa na kuendelea kutumika katika shughuli za utekelezaji wa majukumu ya Halmashauri.

Katika hatua nyingine Mhe. Lucas J. Lemomo amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Bi. Rehema S. Bwasi kwa usimamizi mzuri wa miradi na kwa namna kasi ya utekelezaji wa miradi unavyokwenda haraka hasa ujenzi wa wodi za wanawake, wanaume na watoto katika Hospitali ya Wilaya unaotekelezwa kwa fedha kutoka Serikali kuu kiasi cha shilingi millioni mia tano  pamoja na jengo la ofisi za Halmashauri ambao unatekelezwa baada ya kupokea fedha za awali kiasi cha shilingi millioni mia saba na hamsini.

“Kiukweli hili limenifurahisha niseme tu ukweli kasi mnayokwenda nayo ni nzuri na inaridhisha, niwaombe muongeze spidi zaidi tumalize kabla ya wakati sio lazima kumaliza ndan ya wakati tunaweza kumaliza kabla ya wakati” Mhe. Lucas J. Lemomo amesisitiza alipokuwa akikagua ujenzi wa wodi hizo tatu.

“Lakini pia sikutegemea kukuta hiki kinachoendelea katika eneo la ujenzi wa jengo la Utawala la Halmashauri kwani nilifikiri nitakuta mnasafisha eneo kumbe mmeshafikia hadi uchimbaji tayari kwa kunyanyua nguzo, nawapongeza sana muendelee na hii kasi” ameongezea Mhe. Lucas J. Lemomo wakati wa kukagua ujenzi wa jengo la utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro.

MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 10, 2025
  • TANGAZO A UPANGA VYUMBA VYA OFISI NA MAENEO MBALIMBALI YALIYOPO MOROGORO MJINI March 19, 2025
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • ORODHA YA WANAFUNZI WA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO AWAMU YA PILI 2018. September 07, 2018
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • SHILINGI MILIONI 538 NA LAKI NNE KUNUFAISHA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WALEMAVU

    June 20, 2025
  • MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI: MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 12, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEEA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO,MAAGIZO YATOLEWA

    April 11, 2025
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.