• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Mkuu wa Mkoa Atoa Rai Viongozi wa Mkoa wa Marogogo Kushirikiana

Imetolewa: January 8th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare amewataka viongozi wa ngazi mbalimbali Mkoani humo kushirikiana katika kutatua changamoto zinazowakabili wananchi ili kuwaletea maendeleo.

Sanare ameyasema hayo Januari 7, 2020 wakati akifunga kikao baina yake na watumishi wa ngazi ya Mkoa, Wabunge wa Mkoa huo, Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi kilichoandaliwa kwa lengo la kujadili kwa pamoja kero mbalimbali zinazowakabili wananchi wa Mkoa huo na namna ya kuzitafutia ufumbuzi.

Sanare ameshangazwa na mwenendo wa baadhi ya wabunge wa mkoa huo wa kutoshiriki katika vikao muhimu vinavyoitishwa ngazi ya Mkoa akisema kwamba ndani ya vikao hivyo ndio sehemu wanayoweza kupata kero mbalimbali za wananchi wanaowaongoza na kuziwasilisha bungeni.

Kauli hiyo ya mkuu wa mkoa inakuja, ikiwa tayari ameshatembelea Halmashauri zote za Mkoa huo tangu kuripoti Mkoani humo sambamba na kushiriki katika vikao vikubwa vya kimkoa kikiwemo kile cha Bodi ya Barabara na Kikao cha ushauri cha Mkoa (RCC) huku idadi ya wabunge waliohudhuria ikiwa hairidhishi ukilinganisha na wabunge wote 14 waliopo Mkoani humo.

Ameongeza kuwa katika kutafuta ufumbuzi wa kero za wananchi yapo masuala yanayo hitaji ushiriki wa wabunge moja kwa moja katika utatuzi wake ukiachilia mbali masuala yanayo hitaji kusimamwa kisheria.

Washiriki wa mkutano huo wamepongeza maamuzi ya Mkuu wa Mkoa, wakisema pamoja kikao hicho kimekuja kwa kuchelewa kitasaidia kuweka dira ya mbeleni, ukizingatia viongozi wote kila mmoja ana nafasi yake katika kuwatumikia wananchi.

 

Kikao hicho cha siku moja, kimelenga kuwakutanisha wabunge wote wa Mkoa huu, Wakuu wa wilaya, wakurugenzi na wajumbe wote wa kamati ya ulinzi na usalama, kuweka mikakati ya pamoja kutafuta ufumbuzi wa changamoto kwa wananchi, sambamba na taarifa ya maendeleo katika sekta ya elimu huku Mkuu wa Mkoa akisistiza kufanyika kwa kikaokama hicho kila baada ya kipindi cha robo mwaka kupita.

Na. Andrew Chimesela, Morogoro.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO A UPANGA VYUMBA VYA OFISI NA MAENEO MBALIMBALI YALIYOPO MOROGORO MJINI March 19, 2025
  • TANGAZO LA KAZI YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU, DEREVA NA MTENDAJI WA KIJIJI July 15, 2024
  • TANGAZO LA RASIMU July 25, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 12, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEEA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO,MAAGIZO YATOLEWA

    April 11, 2025
  • KATIBU TAWALA MKOA WA MOROGORO AENDELEZA KAMPENI YA JISOMESHE NA MKARAFU

    March 14, 2025
  • "BAINISHENI VYANZO VYA MAJI NA MVILINDE" MHE.KASSIM MAJALIWA MAJALIWA

    March 05, 2025
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.