• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MOROGORO DC KUTUMIA MILIONI 30 KUANZISHA UHIFADHI MISITU

Imetolewa: May 20th, 2022

HALMASHAURI ya Wilaya ya Morogoro, katika mwaka wa fedha 2022/2023 imetenga Sh. milioni 30 kwa ajili ya kuanzisha Mradi ya Usimamizi Shirikishi wa Misitu (USMJ) katika vijiji vitatu vya Lumbachini, Sesenga na Lubumu.

Halmashauri hiyo inakuja na wazao hilo baada ya kuona mafanikio ya UMSJ katika vijiji vya Matuli, Lulongwe, Diguzi, Mlilingwa na Tununguo ambavyo vimeweza kutekeleza miradi ya maendeleo na jamii.

Wananchi wa Matuli wanatekeleza Mradi wa Kuleta Mageuzi katika Sekta ya Mkaa Tanzania (TTCS), maarufu ‘Mkaa Endelevu’ kupitia wa uwezeshaji wa Shirika la Uhifadhi wa  Misitu ya Asili Tanzania (TFCG) na Mtandao wa Jamii wa Usimamizi wa Misitu Tanzania (MJUMITA) kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Uswis (SDC).

Akizungumzia na wananchi wa kijiji cha Matuli  Mkurugenzi wa Halmashauri, Bi. Rehema Bwasi, amesema mafanikio ya kijiji na wananchi wa Matuli yanawasukuma kuongeza vijiji vipya ili kuchochea maendeleo.

“Tushatupa nduano, kazi yetu ni kwenda kuvua samaki. Tumefundishwa ujanja, basi jukumu letu ni kuhakikisha tunasambaza dhana hii. Hatutegemei mradi huu kufa bali mradi huu utawezesha kusihi kizazi na kizazi.

Sisi halmashauri tumetenga zaidi ya Sh.milioni 30 ili tuweze kuingiza vijiji vitatu vya Lumbachini, Sesenga na Lubumu kwa mwaka huu wa fedha. Tumeona sukari tumeipata Matuli, Diguzi, Lulongwe, Mlilingwa na Tununguo kina mmoja lazima ailambe ilia one utamu wake,” alisema.

Bwasi amesema halmashauri inatarajia kutenga fedha kila mwaka ili waweze kufikia vijiji vyote 149 hasa vile ambavyo vina misitu ya uhifadhi.

Mkurugenzi huyo alisema wamejipanga kuendeleza ushirikiano na TFCG na MJUMITA na wadau wote wa uhifadhi ili kuhakikisha vijiji vyote venye misitu ya asili inachochea maendeleo.

Ofisa Mtendaji wa kata ya Matuli Omary Chombo alisema USMJ katika  kijiji hicho umefanikiwa  kuingizia zaidi ya Sh.milioni 105 ambazo zimewezesha ujenzi wa miradi ya madarasa ya shule ya sekondari na msingi, nyumba ya mganga, zahanati, matundu ya choo.

Pia amesema kupitia mradi huo wameweza kumlipa mlinzi mshahara, kuchimba visima sita vya maji, kukopeshana, kukata Bima ya Afya (CHF) kaya 326 na nyingine.

Chombo alisema pia wametenga fedha kwa ajili ya sekretarieti ya kijiji, posho ya doria hali ambaho inachochea uhifadhi.

“Pia mradi wa TTCS umeboresha elimu na kuchangia ufaulu kuongezeka, hii ni kutokana na kuwepo makambi ambayo yanasaidia wanafunzi kupata chakula,” alisema.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Maliasili kijiji cha Matuli, Sadiki Kondo mradi wa TTCS umefanya mapinduzi makubwa ya kiuhifadhi, mazingira, uchumi na maendeleo kijijini kwao.

Kondo alisema msitu wa hifadhi wa kijiji cha Matuli una ukumbwa wa zaidi ya hekta 1,500 ambapo mradi unatekelezwa katika eneo la hekta 500 na kwa mwaka wanavuna vitalu 66.

“Mradi huu unafuata mzunguko wa miaka 24 baada ya kuvuna kitalu kimoja, hali ambayo kwa miti kama hii ya miombo inakuwa imeota tena kwa ajili ya uvunaji,” alisema.

Meneja Mradi wa Kuhifadhi Misitu kupitia Biashara Endelevu ya Mazao ya Misitu (CoFoReST), Charles Leonard alisema TFCG na MJUMITA wamelazimika kupeleka mpango wa USMJ ili kuokoa misitu ya vijiji kama sheria namba 5 ya ardhi ya 1999 inavyotaka.

“Misitu ya vijiji ilikuwa shamba la bibi, kwani kila mtu alikuwa anaingia anavuna, ila kupitia mradi huu, wananchi wamekuwa walinzi na wasimamizi wa rasilimali misitu, kwani wanapata faida nayo. Mradi unaisha Novemba mwaka huu naomba halmashauri ijipange kuendeleza,” alisema

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 10, 2025
  • TANGAZO A UPANGA VYUMBA VYA OFISI NA MAENEO MBALIMBALI YALIYOPO MOROGORO MJINI March 19, 2025
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • ORODHA YA WANAFUNZI WA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO AWAMU YA PILI 2018. September 07, 2018
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • SHILINGI MILIONI 538 NA LAKI NNE KUNUFAISHA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WALEMAVU

    June 20, 2025
  • MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI: MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 12, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEEA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO,MAAGIZO YATOLEWA

    April 11, 2025
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.