• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MOROGORO KUWA KITOVU CHA UZALISHAJI WA MAZAO YA VIUNGO.

Imetolewa: January 25th, 2024

Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa amesema mkoa wa Morogoro umejipanga kwa ajili ya kilimo cha mazao ya viungo hususani Karafuu ili kuongeza kipato cha Wananchi wa Mkoa huo na taifa kwa jumla sambamba na kurudisha uoto wa asili katika milima ya Urugulu.

Dkt. Mussa Ali Mussa ametoa kauli hiyo Januari 25, 2024 wakati wa kikao cha Wizara ya Kilimo cha kutambulisha mradi wa uzalishaji wa miche ya mikarafuu kilichofanyika  katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro, kikao kilichoratibiwa kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo.


Amesema, kwa kushirikiana na mashirika mengine yakiwemo Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) na Mamlaka ya usimamizi wa Wanyama Pori Tanzania (TAWA) watatoa bure kwa wananchi miche ya mazao ya Viungo ikiwemo miche ya mikarafuu ili waweze kupanda katika milima ya Uluguru zao litakalokuwa rafiki kwao na kusaidia kutunza mazingira ya milima hiyo.

"milima ya Uluguru inakabiliwa na uharibifu wa mazingira kwa kukata miti ovyo, kwa kupanda mazao hayo ya Karafuu itapelekea wananchi kutokata miti hiyo kwa kuwa inawaingizia kipato na wakati huo itahifadhi mazingira". Amesema Dkt. Mussa.


Katika Hatua nyingine Dkt. Mussa amesema kuwa,  Mkoa huo umeanza kujenga maghala ya kuhifadhia karafuu ili kuwa na sehemu moja ya kuuzia zao hilo, na kusaidia Halmashauri ya Wilaya  ya Morogoro kuweza kusimamia na  kukusanya mapato yake vizuri.

Aidha, amesema, Wananchi wameweza kuhamasika na kuanza kupanda miche ya mikarafuu pamoja na kuzalisha miche hiyo si chini ya laki 4, hivyo kama mkoa wanajipanga ili kwenda kununua miche hiyo iliyozalishwa na wananchi na kuigawa kwao ili waipande.


Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi wa Uzalishaji wa Mazao  Wizara ya Kilimo Bi. Beatrice Banzi amesema lengo la kikao hicho inatokana na utafiti uliofanywa na Wizara hiyo siku za nyuma baada ya  Mkoa wa Morogoro kuonesha nia ya kulima zao hilo.


Kwa sababu hiyo wizara ilifanya utafiti na kugundua kuwa sehemu kubwa ya Mkoa huo inaweza kustawisha zao la karafuu hivyo kuongeza kipato cha wananchi na kuhifadhi mazingira kwa sababu miti ya mikarafuu haifyonzi maji.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 10, 2025
  • TANGAZO A UPANGA VYUMBA VYA OFISI NA MAENEO MBALIMBALI YALIYOPO MOROGORO MJINI March 19, 2025
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • ORODHA YA WANAFUNZI WA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO AWAMU YA PILI 2018. September 07, 2018
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • SHILINGI MILIONI 538 NA LAKI NNE KUNUFAISHA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WALEMAVU

    June 20, 2025
  • MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI: MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 12, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEEA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO,MAAGIZO YATOLEWA

    April 11, 2025
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.