• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MWENYEKITI HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO AWATAKA MADIWANI KUFANYA KAZI KWA MAADILI KULETA MAENDELEO

Imetolewa: January 2nd, 2021

WAHESHIMIWA Madiwani wa Halmashauri ya Morogoro, wametakiwa kutambua kuwa ili kuwa na utawala bora wanao wajibu wa kushugulika na changamoto zinazowakabili wananchi kwa kuhakikisha vikao vya kisheria vinafanyika inavyostahiki kwani vikao hivyo ni njia mojawapo ya kushughulika na kero za wananchi lakini pia kujiletea maendeleo katika maeneo yao.

Rai hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, Mhe. Lucas Lemomo, wakati akifungua Mkutano wa Baraza la Madiwani leo Januari 29/2021 katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri hiyo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari, Mhe.Lemomo, amewataka Madiwani kuhakikisha wanasoma kanuni za Halmashauri na taarifa mbalimbali zinazotoka kwa wataalam lakini pia kujenga ushirikiano katika kutatua kero mbalimbali pamoja na kutekeleza maagizo yote yanayotolewa na Serikali Kuu ili halmashauri iweze kwenda vizuri.

Aidha,Mhe.Lemomo,amewataka Madiwani kushirikiana na Halmashauri kuwa na mpango mkakati wa kuandaa master plan ya mji kwani shughuli mbalimbali zitaongeza kupitia ongezeko la watu kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kiuchumi.

"Ndugu zangu dhamana tuliyopewa ni kubwa sana hamjatumwa huko halimashauri kwenda kujinufaisha sisi na familia zetu, twendeni tukayatekeleze yale tuliyoyaahidi ili kurudisha heshima tuliyopewa na wananchi, lazima tuwe kitu kimoja tufanye kazi kama timu na kuongeza vyanzo vya mapato ili tuboreshe miundombinu yetu bila kutegemea ruzuku kutoka Serikali Kuu " Amesema Mhe. Lemomo.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro , Mhe.Hamisi Msangule,amewata Madiwani pamoja na Watumishi wa Halmashauri kumpa ushirikiano wa kutosha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro kusimamia makusanyo na matumizi ya fedha kutoka Serikali Kuu na Halmashauri ili kuleta maendeleo kwa wananchi.


Mhe. Msangule,amesema kuwa dhamana na heshima waliyopewa madiwani na Wananchi ni kubwa mno na isiyoelezeka na jambo ambao anaweza kuahidi katika Baraza hilo ni ushirikiano wa kutosha katika kuleta maendeleo.

""Natambua uchaguzi huu ulioisha tulipitia mambo mengi sana ,lakini sasa uchaguzi umekwisha ni mwendo wa kuchapa kazi sasa twende kuchapa kazi ili turudishe ile heshima tuliyopewa na wananchi wetu kwa kutuchagua " Amesema Mhe.Msangule.

Mwisho, Mhe. Msangule, amemuomba Mkurugenzi wa Halmashauri pamoja na watendaji wote kuhakikisha wanashirikiana kwa ukaribu ili kuhakikisha wanatatua na kumaliza kero zote zinazowakabili wananchi.

Kwa upande wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, Bi. Rehema Bwasi amesema kama viongozi wanao wajibu wa kuweka mazingira bora ya kujifunza kwa ajili ya kizazi Cha Sasa na baadae.

Naye Diwani wa Kata ya Mkambarani, Mhe. Chars Mbona,amempongeza Mkurugenzi wa Halmashauri, Wakuu wa Idara na Vitengo kwa usimamizi mzuri wa miradi kipindi ambacho Baraza la Madiwani lilivunjwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO A UPANGA VYUMBA VYA OFISI NA MAENEO MBALIMBALI YALIYOPO MOROGORO MJINI March 19, 2025
  • TANGAZO LA KAZI YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU, DEREVA NA MTENDAJI WA KIJIJI July 15, 2024
  • TANGAZO LA RASIMU July 25, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 12, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEEA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO,MAAGIZO YATOLEWA

    April 11, 2025
  • KATIBU TAWALA MKOA WA MOROGORO AENDELEZA KAMPENI YA JISOMESHE NA MKARAFU

    March 14, 2025
  • "BAINISHENI VYANZO VYA MAJI NA MVILINDE" MHE.KASSIM MAJALIWA MAJALIWA

    March 05, 2025
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.