• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

PINGA UKATILI WA KIJINSIA KWA KUTOA TAARIFA KWA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA AU KUTEMBELEA OFISI YA MAENDELEO YA JAMII KUPATA MSAADA WA KISHERIA

Imetolewa: December 3rd, 2024

FAHAMU CHIMBUKO LA  KAMPENI YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA  DUNIANI.


Kila mwaka kuanzia Novemba 25 hadi Desemba 10 Dunia hufanya kampeni ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia lengo likiwa ni  kupinga ukatili na kutetea haki za wanawake.

Ukatili wa kijinsia ni kitendo chochote ambacho anaweza kutendewa mwanaume, mwanamke au mtoto na kitendo hicho huweza kumuathiri kimwili au kisaikolojia. Wanawake na watoto ndio wamekua wahanga wakubwa wa kufanyiwa ukatili wa kijinsia.

Toka mwaka 1981, wanaharakati wa haki za wanawake wamekua wakiitumia Novemba 25, kuadhamisha kupinga ukatili ili kuwaenzi wanaharakati wa kisiasa watatu (Mirabal Sisters) ambao waliuwawa mwaka 1960 huko Jamhuri ya Dominika mwaka 1960, kwa amri ya aliyekua kiongozi wa nchi hiyo Rafael Trujillo.

Mwaka 1993 Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lilipitisha Azimio la kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake kwa kuweka mikakati ya kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na wasichana..

Azimio hilo lilipelekea Baraza hilo mwaka 2000 kuweka azimio likitaja rasmi Novemba 25 kua ni Siku ya Kimataifa ya Kutokomeza Ukatili Dhidi ya  Wanawake. Tamko hili lilipelekea serikali , pamoja na mashirika yasiyo  ya kiserikali na taasisi mbalimbali, kuunga nguvu za pamoja na kuandaa shughuli mbalimbali zenye lengo la kuufanya umma kuongeza ufahamu juu ya suala  la kutokomeza ukatili wa kijinsia.

Mwaka 2006, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Awamu ya saba Ndugu Koffi Annan, alitaka Dunia itambue kua ukatili wa Kijinsia dhidi ya wanawake na watoto wa kike limekua tatizo kubwa hivyo aliona kuna haja ya kua na kipindi maalumu cha kampeni ya kupinga ukatili wa kijinsia.  Hivyo ilikubalika kampeni hiyo ianze Novemba 25 ambayo ni Siku ya Kupinga Ukatili wa Kijinsia na kuhitimishwa  Desemba 10 ambayo ni Siku ya Haki za Binadamu Duniani.

Lengo la kampeni hii ni kuongeza ushawishi, kubadilishana taarifa na uzoefu, kujenga uwezo wa pamoja, matumizi mazuri ya rasirimali zinazopatikana na kuunganisha nguvu za asasi za kijamii katika kuhamasisha, kuelimisha, kukemea na kuchukua hatua kwa pamoja ili kupinga ukatili wa kijinsia katika jamii.

Hivyo basi Kampeni ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia inalenga kupaza sauti ili kuongeza uelewa kwa jamii kuhusu athari hasi za ukatili wa kijinsia na njia za kuondokana na unyanyasaji huo katika jamii.

Serikali pamoja na wadau mbalimbali wanaotetea Haki za Binadamu, hufanya shughuli mbalimbali katika kampeni hiyo ikiwemo midahalo mbalimbali ya hadhara au kwenye taasisi  kama vile shuleni na vyuoni

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 10, 2025
  • TANGAZO A UPANGA VYUMBA VYA OFISI NA MAENEO MBALIMBALI YALIYOPO MOROGORO MJINI March 19, 2025
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • ORODHA YA WANAFUNZI WA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO AWAMU YA PILI 2018. September 07, 2018
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • SHILINGI MILIONI 538 NA LAKI NNE KUNUFAISHA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WALEMAVU

    June 20, 2025
  • MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI: MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 12, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEEA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO,MAAGIZO YATOLEWA

    April 11, 2025
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.