• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Rais Magufuli kuweka Jiwe la Msingi Ujenzi wa Mradi wa kufua umeme Rufiji

Imetolewa: July 25th, 2019

Na. Andrew Chimesela, Morogoro

Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli anatarajia kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa Mradi wa kufua umeme kupitia maporomoko ya maji ya mto Rufiji ikiwa ni ishara ya uzinduzi rasmi wa ujenzi wa Mradi huo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 24 katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Waziri wa Nishati  Mhe. Merdadi Kalemani amesema uwekaji wa jiwe la msingi unatarajiwa kufanyika siku ya Ijumaa tarehe 26 Mwezi huu katika eneo la mradi huo ambapo Rais Dkt. John Pombe Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo.

Amesema utekelezaji wa ujenzi wa mradi huo unatarajiwa kuwa na manufaa makubwa katika adhma ya kuipeleka nchi katika uchumi wa kati ambao unategemea kwa kiasi kikubwa uwepo wa nishati ya kutosha hususani katika shughuli za viwandani.

Ameongeza kuwa mradi huo utakaogharimu kiasi cha fedha shillingi Trilioni 6.5 hadi kukamilika kwake unatarajia kuzalisha  Megawati 2115 kiwango ambacho kitakidhi mahitaji ya ujenzi wa uchumi wa viwanda huku ukitarajiwa kukamilika mwaka 2022.

Aidha Waziri Kalemani amesema Tayari mradi huo umeshatumia muda wa miezi saba ya utekelezaji wake tangu ulipoanza mnamo mwezi Disemba mwaka jana ambapo maendeleo yake ni ya kuridhisa hivyo uwekaji wa jiwe la msingi utachochea kasi ya ujenzi wake.

Amesema Mkandarasi wa ujenzi huo alianza kazi rasmi mwezi juni mwaka huu ambapo kwa sasa kazi mbalimbali zinaendelea ikiwemo kuchoronga miamba pamoja na ujenzi wa madaraja katika eneo la mradi.

Amebainisha kwamba mradi huo utakuwa mwarobaini wa kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na matumizi ya kuni na mkaa ambapo mikoa ya Pwani, Morogoro na Iringa imekuwa ikizalizalisha kiwango cha mkaa unaotokana na ukataji wa miti hivyo kuharibu sehemu kubwa ya uoto wa asili.

Awali akimkaribisha Waziri wa Nishati,  Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe amesema tayari vijiji 22 vimeshanufaika katika kipindi hiki cha ujenzi wa mradi huo kwa kuunganishiwa umeme jambo ambalo halikuwa rahisi hapo kabla.

Aidha amewataka wakazi wa Mkoa wa Morogoro kuchangamkia fursa ya ujenzi wa mradi huo kujikwamua kiuchumi kupitia ajira za watu zaidi ya elfu 10 zitakazozalishwa kutokana na mradi huo .

Mradi wa kufua umeme kupitia maporomoko ya maji ya mto Rufiji unatarajiwa kuwa miongoni mwa miradi mikubwa ya kufua umeme Duniani ambapo kwa bara la Afrika utatarajiwa kushika nafasi ya nne ambapo utaambatana na ujenzi wa bwawa lenye ujazo wa mita za ujazo billion 532 ambalo litashika nafasi 60 kati ya mabwawa makubwa 70 duniani ambapo shillingi Trilioni 6.5 zinatarajiwa kutumika mpaka kukamilika kwake  mnamo  mwaka 2022.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO A UPANGA VYUMBA VYA OFISI NA MAENEO MBALIMBALI YALIYOPO MOROGORO MJINI March 19, 2025
  • TANGAZO LA KAZI YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU, DEREVA NA MTENDAJI WA KIJIJI July 15, 2024
  • TANGAZO LA RASIMU July 25, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 12, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEEA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO,MAAGIZO YATOLEWA

    April 11, 2025
  • KATIBU TAWALA MKOA WA MOROGORO AENDELEZA KAMPENI YA JISOMESHE NA MKARAFU

    March 14, 2025
  • "BAINISHENI VYANZO VYA MAJI NA MVILINDE" MHE.KASSIM MAJALIWA MAJALIWA

    March 05, 2025
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.