• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

‎SIKU YA WAZEE MKOANI MOROGORO YAADHIMISHWA, WAZEE WAPEWA HUDUMA ZA AFYA BURE.

Imetolewa: September 10th, 2025

‎

‎Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mhe. Mussa Kilakala, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima, ameongoza maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Kisaki Gomero, Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, tarehe 10 Septemba 2025.

‎

‎Maadhimisho hayo yamehudhuriwa na mamia ya wazee kutoka maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Morogoro ambapo pamoja na kupewa nafasi ya kushiriki kwenye sherehe hizo, walipata huduma za afya bure ikiwemo vipimo vya presha, kisukari, ushauri wa lishe na huduma za uchunguzi wa macho.

‎

‎Katika hotuba yake, Mhe. Kilakala aliwataka wananchi wote kuendelea kuthamini, kuheshimu na kuwajali wazee kwa kuwa ni hazina ya busara na maarifa katika jamii. Alisisitiza kuwa Serikali inaendelea kuboresha huduma za kijamii kwa wazee, ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa huduma za afya bila malipo kwa wazee wote wenye umri wa kuanzia miaka 60 na kuendelea.

‎

‎Baada ya sherehe hizo, wazee walipata fursa ya kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Mwalimu Nyerere na Bwawa la kuzalisha umeme Kwa nguvu ya Maji la Mwalimu Nyerere (JNHP) – ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wao kwa Taifa na kuwapatia muda wa mapumziko ya kijamii na kielimu.

‎

‎Maadhimisho hayo yaliambatana pia na burudani mbalimbali zikiwemo ngoma za asili, maigizo na mashairi ya kuenzi mchango wa wazee katika maendeleo ya jamii.

‎

‎Kaulimbiu ya mwaka huu ni "Wazee ni Nguzo ya Maendeleo – Tuwaenzi, Tuwaheshimu na Kuwatambua."

‎

‎

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 10, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI MOROGORO DC August 30, 2025
  • TANGAZO A UPANGA VYUMBA VYA OFISI NA MAENEO MBALIMBALI YALIYOPO MOROGORO MJINI March 19, 2025
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • ‎SIKU YA WAZEE MKOANI MOROGORO YAADHIMISHWA, WAZEE WAPEWA HUDUMA ZA AFYA BURE.

    September 10, 2025
  • UZINDUZI WA CHANJO NA UTAMBUZI WA MIFUGO HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO

    September 04, 2025
  • "KAHAMASISHENI WANANCHI KUPIGA KURA" Dkt Batilda Burhani

    August 29, 2025
  • RIADHA SHIMISEMITA 2025 MORO DC YATOLEWA HATUA YA FAINALI

    August 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.