• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

TUNAMSHUKURU MHE. RAIS KUPITIA WIZARA YA TAMISEMI KWA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO, TUNAOMBA WIZARA ITUSAIDIA KUTANUA VIFUNGU ILI TUWEZE KUTUMIA FEDHA HIZO KUKAMILISHA MIRADI KWA HARAKA.

Imetolewa: May 13th, 2021

Na. TAJIRI KIHEMBA, Moro Dc

Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro imefanya kikao chake cha Baraza la Madiwani cha Robo ya tatu tarehe 12 Mei, 2021 katika ukumbi wa Pangawe na kujadili mambo mbalimbali kwa mstakabali wa Halmashauri.

Kikao hicho pia kilipata kuhudhuriwa na wageni mbalimbali waalikwa akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Bakari Msulwa, Katibu Tawala wa Wilaya ya Morogoro Bi. Ruth John lakini pia Msaidizi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Ndugu Francis G. Francis kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.

Akimkaribisha Mwenyekiti wa Halmashauri kufungua kikao, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Bi. Rehema S. Bwasi amewashukuru Wakuu wa Idara na Vitengo, Maafisa Tarafa na Wageni waalikwa wote kwa kuudhuria kikao hiki adhimu ambacho kilikuwa kinakwenda kujadili mambo muhimu kwa mstakabali wa Halmashauri ya Wilaya ya Mororgoro.

Akitoa nasaha zake Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mhe. Bakari Msulwa amesema, “Makusanyo yetu bado si ya kutosha lakini nimefurahi tumekuwa tukikaa na Mheshimiwa Mwenyekiti na Mkurugenzi wamezungumzia habari ya kuwa na vyanzo vingine vya mapato, mimi niwaombe sana waheshimiwa madiwani mkitaka mfanikiwe nafikiri maneno mengi na kelele nyingi na mipango mingi ielekezwe kwenye vyanzo vya mapato.”

Lakini pia Mhe. Bakari Msulwa amezungumzia kuhusu Halmashauri kuwekeza katika kutoa Wanasayansi, “Kuna fedha zimetengwa takribani Shillingi mia tatu na sitini millioni zinakwenda katika shule kumi na mbili au kumi na tano hivi, mimi naomba ndugu zangu Waheshimiwa Madiwani tusimamie hili swala na katika eneo ambalo litatuvuruga huko mbele ya safari nimeshaongea na wakurugenzi, mawaziri na baadhi wa viongozi wa Serikali wanataka kufanya ziara ya kufuatilia hayo mambo. Tuhakikishe kuwa hizo fedha zilizotengwa katika maeneo yetu zinafanya kazi, tuwasimamie watendaji, tupige kelele kama kuna haja ya kupiga kelele lakini kubwa zaidi tuhakikishe maabala zetu zinafanya kazi ili sasa kutengeneza mazingira ya vijana wetu kuingia katika mkondo wa sayansi, haitapendeza miaka kumi au ishirini ijayo tunapima matokeo hatuna wanasayansi kutoka katika maeneo yetu kitakuwa ni kitu cha aibu sana, wanasayansi tunawatengeneza ndani ya ukumbi huu. Tukiamua kutengeneza wanasayansi tukiamua kutengeneza wasomi tukitengeneza hatima ya Halmashauri yetu ni sisi tumepewa jukumu mimi naamini timu hii inatosha kuifanya kazi hiyo.”

Kwa upande wa mwakilishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Msaidizi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro ndugu, Francis G. Francis amesema, “Sisi kama Mkoa kwanza tunawasifu ninyi Waheshimiwa Madiwani kwa utendaji mzuri ambao unatendeka sasa hivi, sisi kama ofisi ya Katibu Tawala tulikwenda katika Halmashauri yenu kutizama tatizo la minada nafikiri mna utaratibu mpya wa kuendesha minada katika Halmashauri yenu, tumepita katika Kata ya Duthumi, Tununguo, Mnada wa Diguzi, tumepita na tumeona lakini kwa kuwa utaratibu huo mpya ulikuwa bado haujaanza vizuri tumeshindwa kushauri vizuri sana lakini tunaamini kwamba huenda huo utaratibu mpya mkiusimamia vizuri unaweza ukawa mzuri. Kwa hiyo tunachokisema kwenu ni kwamba muongozo uwepo wa kuendesha huo utaratibu mpya.”

Ndugu Francis G. Francis ameongezea kwa kusema, “Sisi kama Mkoa tumeona tulizungumzie hapa kwani tunaamini lilianzia hapa kwenye Baraza lenu na mkaenda Chalinze kujifunza na sisi tukawasilisha kwa Katibu Tawala kwamba utaratibu unaweza ukawa mzuri ila kitu ambacho tulikiona pungufu kidogo, mnada kama ule unatakiwa uendeshwe chini ya uangalizi wa Polisi kiusalama, kwa hiyo kwa wiki hizi tatu ambazo minada hii imeendeshwa kwa utaratibu mpya Polisi ambao tuliwakuta kule wameenda lakini kulikuwa na utaratibu ambao haukuonyesha kwamba watakuwa sehemu ya malipo, hivyo sisi kama Mkoa tunashauri Polisi wale walipwe na Halmashauri.”

Mwisho Mwenyekiti wa Halmashauri, Mhe. Lucas J. Lemomo ameishukuru Serikali kuu, “Kwa namna ya pekee kabisa niishukuru Serikali Kuu na hasa Ofisi ya Rais TAMISEMI, Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kupitia Waziri wa TAMISEMI na timu yake yote ya Wizara kwa jinsi ambavyo wameweza kutuletea fedha ya ziada zaidi ya ile bajeti yetu kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo, changamoto tunayokutana nayo katika fedha hizi zinazokuja nje ya bajeti ni vifungu vya kutuwezesha kutumia hizi fedha, hivyo tunaomba Wizara ya TAMISEMI kupitia kwa Waziri husika watusaidie kutanua vifungu ili tuweze kukamilisha miradi yetu kabla ya mwaka wa fedha kuisha.”

MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 10, 2025
  • TANGAZO A UPANGA VYUMBA VYA OFISI NA MAENEO MBALIMBALI YALIYOPO MOROGORO MJINI March 19, 2025
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • ORODHA YA WANAFUNZI WA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO AWAMU YA PILI 2018. September 07, 2018
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • SHILINGI MILIONI 538 NA LAKI NNE KUNUFAISHA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WALEMAVU

    June 20, 2025
  • MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI: MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 12, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEEA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO,MAAGIZO YATOLEWA

    April 11, 2025
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.