• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WAH: MADIWANI HALMASHAURI YA MOROGORO WATEMBELEA BANDA LA HALMASHAURI YA MOROGORO

Imetolewa: August 8th, 2022

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya Morogoro, Mh Lucas Lemomo pamoja na timu ya madiwani hapo jana, wametembelea katika mabanda ya maonesho ya kilimo ya Halmashauri ya wilaya hiyo, yaliyofanyika katika viwanja vya maonesho ya kilimo na mifugo vya mwalimu Julias Kambarage Nyerere mjini Morogoro, na kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na wananchi wa Halimashauli hiyo.

Mh Lemomo, ametoa pongezi kwa Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bi Rehema Bwasi pamoja na timu nzima iliyohusika katika maandalizi ya maonesho hayo, kwa kujipanga vizuri katika kutoa elimu stahiki kwa wakulima, wafugaji na wafanyabiashara, ili waweze kulima na kufuga kwa kufuata kanuni na taratibu na kupata matokeo chanya na kuendeleza kukuza uchumi wa nchi.

Pia katika maonesho hayo, wananchi pamoja na wageni waliotembelea katika Halimashuri hiyo, wamefundishwa namna kuhifadhi na kuitunza milima ya Ulugulu inayopatikana katika Halmashauli hiyo namna ya kulima na kupanda miti inayotoa faida ikiemo miti ya viungo ikiwa ni njia mojawapo ya kuendelea kuitunza na kuhifadhi milima hiyo.

 Rashid Athuman mkazi wa Tuliani katika wilaya ya Morogoro amefurahishwa na ukarimu wa watendakazi wa Halimashauri hiyo kwa kumfundisha juu ya kilimo endelevu cha miti ya viungo ambapo kilimo hicho kitamwezesha kulima mazao hayo pasipo kuikata miti mingine na kuharibu mazingira

Kadhalika Diwani wa kata ya Mkuyuni iliyopo katika Halimashauri hiyo Mhe Asha Ally Almasi amefurahishwa na mafunzo yaliyotolewa katika Halmashauri hiyo hasa katika sekta ya kilimo ambapo alijifunza namna ya kufuga na kulima kisasa na kupata matokeo makubwa

Aidha maadhimisho ya maonesho ya kilimo maarufu kama nanenane huadhimishwa mwezi augost kila mwaka ambapo sekta mbalimbali hukusanyika katika kila kanda na kuonesha shughuli mbalimbali wanazozifanya ikiwa ni njia mojawapo ya kujitangaza na kutoa elimu kwa wananchi na wageni wanaotenbelea maadhimisho hayo.

Maadhimisho hayo yalifunguliwa rasmi  tangu August 1, 2022 na waziri mkuu mstaafu Mh Mizengo Pinda katika viwanja vya maonesho ya kilimo vya mwalimu Julias Kambarage Nyerere vilivyopo katika kata ya Tungi Manispaa ya Morogoro nakuhitimishwa hapo jana August 08,2022 ambapo kitaifa maadhimisho hayo yamefanyika jijini Mbeya.

Na mwandishi Atusa Laurence Bukuku

                                                                                         

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO A UPANGA VYUMBA VYA OFISI NA MAENEO MBALIMBALI YALIYOPO MOROGORO MJINI March 19, 2025
  • TANGAZO LA KAZI YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU, DEREVA NA MTENDAJI WA KIJIJI July 15, 2024
  • TANGAZO LA RASIMU July 25, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 12, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEEA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO,MAAGIZO YATOLEWA

    April 11, 2025
  • KATIBU TAWALA MKOA WA MOROGORO AENDELEZA KAMPENI YA JISOMESHE NA MKARAFU

    March 14, 2025
  • "BAINISHENI VYANZO VYA MAJI NA MVILINDE" MHE.KASSIM MAJALIWA MAJALIWA

    March 05, 2025
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.