• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WAZAZI NA WALEZI LUNDI WAPEWA ELIMU YA LISHE KWA VITENDO

Imetolewa: September 23rd, 2024

Wazazi na walezi wenye watoto chini ya umri wa miaka mitano wa kijiji cha Muungano kata ya Lundi halmashauri ya wilaya ya Morogoro  wamepewa elimu ya afya,ikiwa ni  utayarishaji, upishi wa vyakula na ulishaji kwa watoto wachanga na watoto wadogo kwa kuzingatia aina ya vyakula ambavyo watoto wanapaswa kula. lengo la elimu hiyo ni kuimarisha ukuaji, maendeleo na Afya ya mtoto.

Hayo yalijiri wakati wa maadhimisho ya Siku ya Afya na Lishe ya Kijiji (SALiKi) katika kijiji hicho yaliyofanyika Septemba 23, 2024 ambapo watu mbalimbali walishiriki ikiwa ni pamoja na wazazi/walezi wenye watoto chini ya miaka mitano, viongozi wa kijiji, wahudumu wa afya ngazi ya jamii na watumishi kutoka Hospital ya Wilaya.

Baadhi ya wazazi na walezi wa kijiji cha Muungano kata ya Lundi wakipata chakula cha lishe baada ya kupatiwa elimu kwa vitendo katika maadhimisho ya SALiki.jpg

Shughuli mbalimbali zilifanyika ikiwa ni pamoja na utoaji wa elimu ya Lishe, elimu ya Afya na umuhimu wa chanjo pamoja na kupima hali ya Lishe na kutoa chanjo kwa watoto chini ya miaka mitano. .  Aidha, wazazi na walezi walioshiriki walipata elimu ya uandaaji wa chakula cha watoto kwa njia ya mapishi kwa vitendo yaliyoongozwa na wahudumu wa Afya ngazi ya Jamii.

Akitoa eimu ta lishe mhudumu wa afya bgazi ya jamii Bw. Msafiri Ngomeka amewasisitiza wazazi/walezi kuwapa watoto chakula ambacho ni mlo kamili kwa kuzingatia makundi ya vyakula ambayo ni nafaka, mizizi,ndizi mbichi kwa ajili ya kuupatia mwili wa mtoto nishati lishe (Wanga ) au nguvu, vyakula vya asili ya wanyama na  vyakula vya jamii ya kunde ambavyo huupatia mwili protini kwa ajili ya ukuaji na kujenga afya njema, mbogamboga na matunda kwa ajili ya kupata vitamini na madini ambayo humkinga mtoto na maradhi na kuwezesha mwili wa mtoto kufanya kazi kwa ufanisi.     Pia amesisitiza ni muhimu kuhakikisha wazazi wanawapa vyakula mchanganyiko kwa kuzingatia na kutumia vyakula vinavyopatikana katika mazingira yetu ambavyo ni rahisi na sio gharama

Sambamba na hayo watoto takribani 70 wamepimwa hali ya lishe (uzito kwa umri) na hakuna aliyekutwa na changamoto ya uzito pungufu.

Aidha watoto chini ya miaka mitano wamepatiwa dawa za minyoo na vitamini A. Ambapo watoto jumla ya watoto 14 walipata chanjo watoto 46 wenye umri kuanzia mwaka 1-5 walipatiwa vitamini A na dawa za minyoo.

Wananchi wa Lundi wameshukuru kwa kupatiwa elimu na hamasa ya uzingatiaji wa lishe bora haswa wakikumbushwa kuwa makundi yote saba ya vyakula vikiwepo na vile vya asili vinapatikana kwa urahisi katika maeneo yao.

Siku ya Afya na Lishe ya Kijiji (SALiKi) ni siku maalum inayoadhimishwa mara moja kila robo ya mwaka katika ngazi ya kijiji kwa lengo la kuhamasisha masuala ya afya na lishe. siku hii ni mpango jumuishi wa kuboresha upatikanaji wa huduma za afya na lishe kwa mama na mtoto katika ngazi ya jamii, na utekezaji wake  ni mojawapo ya afua maalum inayoweza kuchangia kupunguza matatizo ya lishe duni kwa watoto wachanga na jamii.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 10, 2025
  • TANGAZO A UPANGA VYUMBA VYA OFISI NA MAENEO MBALIMBALI YALIYOPO MOROGORO MJINI March 19, 2025
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • ORODHA YA WANAFUNZI WA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO AWAMU YA PILI 2018. September 07, 2018
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • SHILINGI MILIONI 538 NA LAKI NNE KUNUFAISHA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WALEMAVU

    June 20, 2025
  • MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI: MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 12, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEEA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO,MAAGIZO YATOLEWA

    April 11, 2025
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.