• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Morogoro District Council
Morogoro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Afya
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Vijana
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Utalii
    • Vivutio vya Utalii
      • Msitu wa Pangawe
      • Msitu wa Milawilila
      • Msitu wa Kimboza
      • Maji Moto-Kisaki
      • Kisimbi-Kinole
      • Utalii Matombo
    • Maeneo ya Kihistoria
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Huduma za Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

ZOEZI LA UPIMAJI VIWANZA LAZINDULIWA KISAKI

Imetolewa: February 24th, 2022

Na. Tajiri Kihemba,  MOROGORO DC.

Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro imezindua zoezi la upimaji wa viwanja katika Kijiji cha Kisaki Kituoni ikiwa ni hatua ya utekelezaji wa Mradi wa Kupanga, Kupima na Kumilikisha ardhi katika Miji katika Halmashari ya Wilaya ya Morogoro.

Uzinduzi huo umefanyika jana Februari 24, 2022 na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, Mhe. Lukas J Lemomo kwenye Mkutano wa Wananchi kijijini hapo.

Akizungumzia lengo la Serikali katika kupanga na kupima eneo la Kisaki, Mkuu wa Idara ya Ardhi Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, Ndugu Patrick Mwakilili amesema kuwa Serikali ina lengo la kuwezesha ukuaji endelevu wa makazi na shughuli za kiuchumi zitakazochochewa na mradi wa Bwawa la umeme la Mwalimu Nyerere pamoja na Hifadhi ya Taifa ya Nyerere.

Viwanja 3,888 vya matumizi mbalimbali vinatarajiwa kupimwa na mradi huu unalenga makundi yafuatayo;

1. Wananchi wa kawaida kwa ajili ya kupata viwanja vya kujenga nyumba bora za makazi.

2. Wafanyabiashara kwa ajili ya kuweka biashara mbalimbali kama maduka, nyumba za kulala wageni na nyinginezo.

3. Wawekezaji kwa ajili ya kupata viwanja vya matumizi ya viwanda vidogo, hotel, kambi za kitalii, Elimu na uwekezaji mwingine.

4. Taasisi mbalimbali kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi.

Upimaji uliridhiwa na kupata Baraka za Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro ufanyike upimaji shirikishi wa viwanja kwa awamu kwa kugawana viwanja na wamiliki wa maeneo kwa uwiano wa asilimia 60 (Mwananchi) kwa asilimia 40 (Halmashauri ya Wilaya).

Asilimia 40 ya ardhi inayokwenda Halmashauri ya Wilaya ndio gharama ya kupima maeneo na kuweka miundombinu muhimu kama barabara, makaravati na miundombinu mingine ikiwa ni pamoja na kurudisha Mkopo wa fedha ambayo Halmashauri imekopa kwa ajili ya upimaji wa viwanja hivyo.

Kwa kuanzia, Halmashauri itapima viwanja 2,500 kwa kutumia makampuni ya upimaji ili kuharakisha upimaji na upimaji huo utaendelea kwa awamu hadi hapo eneo lote lililopangwa litakapopimwa lote.

Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro inatarajia kutangaza bei ya viwanja hivyo muda mchache baada ya kukamilika kwa zoezi la upimaji.

#KisakiNaNgerengereKuwaMijimidogo

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 10, 2025
  • TANGAZO A UPANGA VYUMBA VYA OFISI NA MAENEO MBALIMBALI YALIYOPO MOROGORO MJINI March 19, 2025
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • ORODHA YA WANAFUNZI WA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO AWAMU YA PILI 2018. September 07, 2018
  • Angalia zote

Habari za hivi karibuni

  • SHILINGI MILIONI 538 NA LAKI NNE KUNUFAISHA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WALEMAVU

    June 20, 2025
  • MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI: MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 12, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEEA HALMASHAURI YA WILAYA YA MOROGORO,MAAGIZO YATOLEWA

    April 11, 2025
  • Angalia zote

Video

Mfumo wa Mikopo ya 10% Namna ya Kujisajili
Vidio Zaidi

Kurasa za haraka

  • Sheria ya Manunuzi ya umma
  • Sheria ya Ardhi

Tovuti nyingine

  • Salary Slip Self Service
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani yake

Wasiliana nasi

    Mvuha Area, 450M- Bigwa-Kisaki Road

    Sanduku la barua: 1880, Morogoro Tanzania

    Simu: +255 23 2935458

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: ded@morogorodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 H/W Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa.